• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

MADHARA YA LISHE DUNI NI HATARI KWA MTOTO-KWITEGA

Posted on: August 1st, 2020

“Athari za lishe duni kwa watoto ndani ya siku 1000, madhara yake huwa yanatokea kwenye maisha yake yote”.

Yamesemwa hayo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha bwana Richard Kwitega,alipokuwa akifungua kikao cha tathimini ya lishe cha nusu mwaka kwa Mkoa wa Arusha.

Amesema madhara ya lishe duni huwa ni makubwa sana kuliko jamii inavyoelewa hasa kwa watoto wadogo na wajawazito.

Ametaja baadhi ya athari hizo kuwa ni udumavu, kuvimba tezi la shingo, upungufu wa damu, upungufu wa madini ya chuma mwilini hasa kwa wajawazito na kupata vidonda mdomoni.

Amesema serikali ya awamu ya tano imeweka nguvu kubwa katika kuhakikisha hali ya lishe nchini inaimarika kwa kiwango kikubwa ili kuiwezesha nchi kuingia katika uchumi wa kati.

Kwitega amesisitiza kuwa ili hali ya lishe katika mkoa wa Arusha iweze kuimarika zaidi elimu itolewa kuanzia ngazi ya familia kupitia kwa waratibu wa lishe wa jamii.

Hivyo amezitaka halmashauri zote za Mkoa wa Arusha kuhakikisha wanatenga shilingi 1000 kwa kila mtoto wa chini ya umri wa miaka 5, ili fedha hizo zikasaidie kuongeza utoaji wahuduma za lishe katika ngazi zote.

Nae, afisa lishe Mkoa wa Arusha bi.Anna  Andrew, amesema hali ya udumavu katika mkoa wa Arusha imeshuka kutoka asilimia 36 mwaka 2014  hadi asilimia 25.5 mwaka 2018 sawa na Watoto 75,959 walio katika mpango wa siku 1000 za lishe bora.

Amesema katika darasa lenye watoto 45 watoto 14 wana udumavu hivyo kupelekea kushindwa kufundishika.

Aidha, amesema changamoto kubwa inayosababisha hali ya udumavu kuendelea kuwepo katika Mkoa ni elimu duni kwa watoa huduma za lishe ngazi ya jamii na baadhi ya jamii kutowaibua watoto wenye udumavu.

Akitoa mikakati ya kupunguza udumavu katika Mkoa wa Arusha, Mganga Mkuu wa Mkoa Daktari Wedson Sichalwe, amesema mkoa utaendelea kusimamia hali ya lishe kwa wamama wajawazito na watoto kwa ukaribu zaidi, huku wakitoa elimu ya kutosha kwa watoa huduma za lishe ngazi zote.

Pia,Kutoa matibabu kwa wagonjwa watakaogundulika na ukondefu mkali na kuendelea kuhamasisha jamii kutumia chumvi ya madini joto ili kuongeza madini mwilini zaidi.

Kikao cha tathimini cha lishe kwa Mkoa wa Arusha hufanyika mara 2 kwa mwaka kwa lengo la kujadili hali halisi ya lishe kwa Mkoa na kubaini changamoto zilizojitokeza kwa kipindi hicho.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO KIDATO CHA NNE,KIDATO CHA PILI NA DARASA LA NNE. January 15, 2021
  • KERO ZA WANANCHI KUSIKILIZWA KILA SIKU July 14, 2020
  • MATOKEA YA DARASA LA SABA 2020 November 21, 2020
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 18, 2020
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • SITAKI UFAULU WA DARAJA LA ZERO MKOANI KWANGU

    January 08, 2021
  • RC KIMANTA, BEBENI SIFA YA NCHI ZAIDI KULIKO BINAFSI

    December 19, 2020
  • WAMILIKI WA SHULE MKOANI ARUSHA WAMETAKIWA KUFUATA MIONGOZO YA UWENDESHAJI WA SHULE

    December 19, 2020
  • CHANGIENI TIMU YA MKOA

    December 17, 2020
  • Angalia Zote

Video

HAKUNA DIVISION ZERO ARUSHA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Sanduku la Barua: 3050 Arusha

    Simu: 27 254 5608

    Simu Nyingine: 027 254 4950

    Barua Pepe: ras@arusha.go.tz

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa