• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

107 Wamiliki Pikipiki

Posted on: March 6th, 2018

Waendesha bodaboda mkoani Arusha wapewa miezi mitatu kuhakikisha wanajifunza sheria na taratibu za barabara bila kusumbuliwa na polisi wa barabarani.

Akitoa kauli hiyo,Waziri wa mambo ya ndani mheshimiwa Mwigulu Nchemba katika kikao chake na waendesha bodaboda wa mkoa wa Arusha alipokuwa akiwagawia kadi za umili wa bodaboda  kwa madereva 107 waliofanikiwa kumaliza mkopo wa mradi wakukopesha pikipiki ulioanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Kauli hiyo imetolewa na mheshimiwa waziri baada ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha kutoa ombi maalum kwake lakuwaruhusu madereva bodaboda hao kujifunza sheria kwanza kisha ndio polisi waanze utaratibu wakuwakamata wale wote watakaokuwa wamekiuka sheria za barabarani.

Mwigulu Nchemba amewasihi bodaboda wote nchini kuchukulia hii kazi kama yenye heshima ili iweze kuwabadilisha maisha yao na tegemeze wao.

Aidha,amesisitiza utoaji wa leseni kwa bodaboda utazingatia kwa wale ambao watakuwa wanamiliki kofia mbele na hata akiwa na cheti pia atapatiwa leseni,pia abiria atakaekaidi kuvaa kofia basi atapatiwa adhabu yeye nasio dereva kama ilivyokuwa awali.

Akichangia zaidi juu ya mradi huu,Mwiguli Nchemba atachangia kiasi cha shilingi milioni 10 ilikusaidia vijana wengine waweze kukopeshwa pikipiki kwa wingi.

Pia, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo,amewaambia bodaboda kuwa wanaweza kutumika katika kubeba watalii ikiwa tu wataweza kufuata sheria na taratibu za barabarani.

Amewapongeza watendaji kata na maafisa tarafa wa Jiji la Arusha kwakuonyesha ushirkiano mkubwa katika kufanikisha makusanyo na kwa wakati, na kiasi cha shilingi milioni 306 tayari zimesharudishwa na milioni 200 zitatumika kukopesha wamama wajasiriamali wadogo kwa mkopo wa shilingi laki 2 kwa wamama 500.

Amesema kiasi cha pesa kinachobaki cha zaidi ya milioni 100 kitatumika kukopesha waendesha bodaboda wengine,hii itasaidia kuwawezesha vijana wengi kumuliki pikipiki zao wenyewe badala yakutegemea pikipiki za watu wengine ambazo zinawabana sana.

Kamanda wa polisi kitengo cha barabarani Joseph Buberwa,amewataka bodaboda kuhakikisha wanatii sheria bila shuruti,wapunguze spidi barabarani hususani kwenye makazi ya watu.

Amesema kuwa polisi barabarani hawatawakamata bodaboda ambao hawana leseni lakini wana cheti cha udereva na watawapa mda wakuhakikisha wanapata lesenina amewapongeza madereva 250 waliofanikiwa kuhitimu mafunzo ya udereva.

Akisisitiza zaidi mwenyekiti waumoja wa madereva bodaboda (UBOJA) bwana Mauridi Makongoro,amesema mradi huo umewanufaisha sana bodaboda wengi kwani umewatoa katika mazingira yakuendesha bodaboda za watu wengine na sasa wanamiliki zao wenyewe na wameweza kuingiza kipato chakutosha.

Mradi huu ulianzishwa mwaka 2017 na mheshimiwa Gambo kwa lengo lakuwakwamua bodaboda wa Jiji la Arusha katika changamoto yakukosa mtaji wakumiliki pikipiki zao, vijana  200 walifanikiwa kukopeshwa pikipiki hizo na kati yao 107 wamemaliza mkopo nakukabidhiwakadi za umiliki wa pikipiki na wengine wanaendelea na marejesho.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa