• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

BILIONI 2.5 KULIPA FIDIA WATAKAOPISHA UJENZI WA UWANJA WA MPIRA ARUSHA...

Posted on: December 18th, 2023

Na Elinipa Lupembe.


Kufuatia mkakati wa Serikali ya awamu ya sita, wa kujenga uwanja wa mpira wa miguu, ikiwa ni maandalizi ya mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), yanayotarajiwa kufanyika mapema mwaka 2027, Halmasahuri ya Jiji la Arusha, imetenga Shilingi Bilioni 2.5 kwa ajili ya kulipa fidia wananchi watakayotoa maeneo yao.


Akitoa taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo, kwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Damas Damian Ndumbaro ( MB), Mkurugenzi Mtendaji, Jiji la Arusha, Mhandisi Jumaa Hamsini, amesema kuwa Serikali ilitoa maagizo ya kupatikana Eka 83 na mpaka sasa tayari zimepatikana Eka 39, zikiwa zimeandaliwa Hati Miliki, huku Jiji la hilo likitenga shilingi Bilioni 2.5, kwa ajili ya kulipa fidia wananchi watakaopisha maeneo kwa ajili ya ujenzi wa uwanja huo wa mpira.


Amesema kuwa, tayari hatua zote zimeshafanyika, na Jiji limetenga kiasi hicho cha fedha, ambacho kitatumika kulipa fidia kwa wananchi ili kupata eneo la Eka 44 zitakazokwenda kukamilisha Eka 83 zinazotakiwa na Serikali ili kutekeleza ujenzi huo.


"Sisi kama Jiji la Arusha, tumeshajipanga vema, kuhakikisha adhma ya Serikali ya awamu ya sita, inafikiwa kwa kiwa na uwanja wa mashindano, viwanja vya mazoezi pamoja na miundombinu yote inayohitajika inajengwa hapa Mtaa wa Murongoine kata ya Olmoth na tutahakikisha mashindano hayo yatafanyika kama yalivyopangwa".Ameweka wazi Mhandisi Hamsini.


Awali, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, ametembelea na kukagua eneo linaloandaliwa kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa mpira na viwanja vya mazoezi, na hatimaye Jiji la Arusha kumkabidhi mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. John V.K Mongella Hati Miliki ya Eka 39 na Kumkabidhi Waziri huyo mwenye dhamana.


Ikumbukwe kuwa ujenzi wa uwanja wa mpira wa kimataifa mkoani Arusha, licha ya kuwa ni kwa ajili ya mashindano ya kimataifa ya AFCON lakini zaidi ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi unaokwenda kuwekeza kwenye utalii wa michezo katika mkoa wa Arusha na Tanzania kwa ujumla wake.


#arushafursalukuki


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa