• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA CHATAKIWA KUWEKEZA KWENYE TEKNOLOJIA YA KISASA

Posted on: January 15th, 2024


Na Daniel Gitaro

Chuo kikuu Huria cha Tanzania (OUT) kimetakiwa kuwekeza zaidi kwenye teknolojia ya kisasa, katika utoaji wa elimu ili kuendana na kasi ya ulimwengu wa sasa ambao umejikita zaidi kwenye mifumo ya kiteknolojia.


Rai hiyo, imetolewa na Mkuu wilaya ya Arusha Mhe. Felician Mtahengerwa, wakati akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John V.K Mongella, wakati wa mahafali ya 42 ya chuo hicho, yalifanyika kwenye viwanja vya chuo hicho Kampasi ya Mkoa wa Arusha.


Mhe. Mtahengerwa, amesema kuwa, kutokana na maendeleo ya Sayansi na teknolojia, uongozi wa chuo hicho, kuwekeza kwenye teknolojia ya kisasa ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya dunia ya kisayansi.


Aidha, licha ya kuupongeza uongozi wa chuo hicho kwa elimu wanayoitoa sambamba na wahitimu katika kada mbalimbali, amewataka wahitimu hao kutumia elimu waliyoipata kuleta mabadiliko chanya katika maeneo yao ya kazi pamoja na kuchochea jitihada za kuleta maendeleo na mapinduzi katika Nchi yetu.


"Nendeni mkaitumie elimu hii mliyoipata hapa kuleta mapinduzi makubwa ya kimaendeleo katika sehemu zenu za kazi na kuleta mabadiliko kwenye jamii na Watanzania wote kwa ujumla". Amesisitiza.


Akisoma risala ya wahitimu, mhitumu wa shahada ya uzamili kitivo cha maktaba na usimamizi wa habari, Rafiki Kilonzo amebainisha kuwa chuo hicho kimekuwa ni fursa kwa wanafunzi kujiendeleza katika ngazi zote za elimu na kuwawezesha wahitimu kufikia malengo yao kwa ufanisi mkubwa zaidi.


Ameongeza kuwa, licha ya mchango mkubwa unaotolewa na chuo hicho, bado kinakabiliwa na changamoto kadha wa kadha ikiwemo baadhi ya wanafunzi kutokuwa na miundombinu rafiki kama vile teknolojia ya TEHAMA, habari na mawasiliano pamoja na uchumu mdogo unaopelekea baadhi kushindwa kumaliza masomo yao kwa wakati.


"Tunaomba viongozi wa Sekta ya walimu wazidi kutoa ushirikiano kwa walimu kwa kuweka mazingira wezeshi zaidi kwa walimu wakati wa mafunzo ya vitendo ili elimu hii iweze kuwafikia na vijana wenzetu popote walipo". Amesema.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa chuo hicho, Dkt. Nangwale Msofe amesema kuwa chuo hicho kimeongeza fursa ya upatikanaji wa elimu Mkoani Arusha kwani tangu kuanzishwa kwake kimehudumia wanafunzi zaidi ya 7500.


Aidha ametumia fursa hiyo kuipongeza na kuishuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuwezesha mradi wa Hit project ambao umewezesha wanafunzi 300 kusoma nje ya nchi kwa mwaka wa masomo 2021/2022 jambo ambalo limechagiza ongezeko la udahili wa wanafunzi kituoni hapo.


"Tunamshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia mradi huo unaosimamiwa na Benki kuu ya Tanzania kupitia Wizara ya Elimu wenye madhumuni ya kutengeneza na kung'arisha mazingira ya ufundishaji kwa elimu ya juu na kufadhili ujenzi wa maabara ya sayansi na ofisi ya kituo cha Arusha". Amesema Mkurugenzi huyo.


Awali, jumla ya wanafunzi 241 wamehitimu masomo yao kwa ngazi tofauti tofauti ikiwemo shahada ya uzamivu (phd), shahada ya uzamili, shahada ya kwanza, stashahada pamoja na astashahada.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa