• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

DIWANI WA KATA YA KIUTU NI MFANO WA KUIGWA; ATOA ENEO LA UJENZI WA SHULE

Posted on: October 3rd, 2024


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amewataka Waheshimiwa Madiwani nchini kuiga mfano wa Diwani wa Kata ya Kiutu Mhe. Malaki Malambo aliyetoa kiwanja chenye ukubwa wa zaidi ya mita za mraba 6,400 kwa ajili ya kujenga shule ya Sekondari Kiutu Halmashauri ya Wilaya ya Arusha.



Mhe. Mchengerwa ametoa wito huo kwa madiwani wote nchini, akiwa kwenye ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua na kuhimiza utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri za Mkoa wa Arusha.



Amesisistiza kuwa, kitendo cha Diwani wa Kata ya Kiutu Mhe. Malambo kutoa kiwanja chake ni ishara ya upendo wa dhati alionao kwa wananchi ambao walimchagua ili awaongoze na kuwaletea maendeleo.



“Ninawaomba Madiwani nchini wengine kuiga mfano mzuri wa Mhe. Malambo aliyejitoa kwa wananchi wake kwa kutoa kiwanja kilichowezesha ujenzi wa shule ya Sekondari Kiutu, hii ndio uhalisia wa kuwatu’ikia wananchi". Amesisitiza.



Ili kuunga mkono jitihada wa Mhe. Malambo na wakazi wa mkoa wa Arusha, Waziri Mchengerwa ameanisha kuwa Ofisi ya Rais-TAMISEMI itafanya mchakato wa kuwezesha kukamilisha ujenzi wa jengo la Shule ya Kiutu ili shule hiyo mwakani ipokea wanafunzi zaidi ya 500 tofauti na mwaka huu ambapo imepokea wanafunzi 400. 



Mhe. Mchengerwa amesema majengo 8 yaliyokamilika hayawezi kuchukua wanafunzi zaidi ya 400, hivyo kuna uhitaji mkubwa wa kukamilisha majengo yaliyosalia ili wanafunzi wapate miundombinu bora na rafiki ya kuwawezesha kutimiza ndoto zao.



“Nikihitimisha ziara yangu, Mkurugenzi wa Idara ya Elimu Ofisi ya Rais-TAMISEMI aje na timu yake kufanya tathmini ya gharama zinazohitajika ili tuwasilishe ombi la fedha kwa Mhe. Rais na hatimaye tuweze kukamilisha ujenzi wa shule hiyo,” Mhe. Mchengerwa amehimiza.



Waziri Mchengerwa yupo mkoani Arusha kwa ajili ya ziara ya kikazi iliyolenga kukagua miradi ya maendeleo na kuhimiza uwajibikaji kwa wasimasmizi wa miradi hiyo ili iweze kukamilika kwa wakati.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa