• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI YA KARATU YAFURAHISHWA NA MAONESHO YA KARIBU KILI FAIR 2024....

Posted on: June 9th, 2024

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Mkoani Arusha Ndugu Juma Hokororo amesema Maonesho ya kimataifa ya Utalii ya Karibu Kili Fair 2024 yamekuwa ni fursa muhimu ya kuwakutanisha na wadau mbalimbali wa utalii katika kuhamasisha zaidi uwekezaji kwenye sekta ya Utalii wilayani Karatu.

Hokororo ametoa kauli hiyo wakati alipotembelea mabanda mbalimbali ya utalii kwenye Viwanja vya Magereza Kisongo leo Juni 09, 2024 akiambatana na Maafisa kadhaa wa Halmashauri hiyo wanaohusika na Utalii, ikiwa ni Kilele cha Maonesho hayo ya Utalii ya Kimataifa.

Hokororo amesema Wilaya ya Karatu inanufaika sana na sekta ya Utalii kutokana na kuwa lango la Utalii wa Arusha kutokana na eneo hilo kuwa njia ya kuelekea kwenye hifadhi za Ngorongoro na Serengeti na hivyo suala la Utalii wamelipa kipaumbele kikubwa katika kuhakikisha dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan inatekelezeka kikamilifu.

"Tangu Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan atengeneze ile filamu ya The Royal Tour tumeona kuanzia mwaka jana Halmashauri ya Wilaya ya Karatu iliweza kupokea wageni wengi sana na hata mapato.Nilifika Karatu mapato ya Service levy yalikuwa Milioni 500 lakini kwa mwaka huu tunategemea kukusanya zaidi ya Bilioni moja kwenye eneo la service levy peke yake." Ameongeza Hokororo.

Akizungumzia tija ya Utalii katika Wilaya hiyo, Mkurugenzi huyo amesema kwa kiasi kikubwa makusanyo yanayotokana na utalii mengi yamekuwa yakielekezwa kwenye maendeleo ya miundombinu na sekta nyingine za kijamii katika kuhakikisha wananchi wananufaika na maendeleo.

Katika hatua nyingine Hokororo amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda kwa kuwa na msukumo mkubwa wa kukuza Utalii Arusha akiahidi kuendelea kushirikiana nae katika kuhakikisha maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan yanatimia kwa mkoa wa Arusha. @halmashauri_ya_karatu @ikulu_mawasiliano @kilifair @hokororojuma


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa