• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

HAYA NDIO MAENEO MACHINGA HAWARUHUSIWI KUFANYABIASHARA

Posted on: September 18th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.John Mongella ametoa mwelekeo wa maeneno ambayo wafanyabiashara wadogo(Machinga) hawatatakiwa kufanya biashara zao.

Ameyasema hayo alipokutana na kufanya kikao na viongozi wa wamachinga, wafanyabiashara na watumishi wa Jiji la Arusha, katika ukumbi wa Ofisi yake.

Ameyataja maeneo hayo kuwa ni maeneo ya ndani ya soko la Kilombero na soko kuu wamachinga hawatakiwi kuwepo ndani ili kuruhusu wateja kuingia na kutoka kwa urahisi.

Pia, amemuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Dkt. John Pima kuhakikisha soko la Muromboo linapangiliwa vizuri na machinga wasizibe Barabara.

Maeneo mengine ni nje ya maduka, kwenye kuta za Hospitali, vituo vya Afya na mashule yanatakiwa kuwa wazi, ili kuruhusu shughuli za maeneo hayo zifanyike kwa umakini zaidi.

Wamachinga wanatakiwa kupisha maeneo ya mitaro inayopitisha Maji na hifadhi zote za Barabara ili kiwawezesha waenda kwa miguuu kupita kwa urahisi.

RC Mongella amesema lazima Mkoa wa Arusha urudi katika hali yake ya zamani yenye mpangilio na kupendeza na ili hayo yote yawezekane ushirikiano ndio silaha muhimu na Jiji la Arusha ndio sura nzima ya Mkoa.

Akibainisha maeneo mapya yaliyopendekezwa kwa ajili ya masoko ya Machinga, Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Dkt John Pima, amesema maeneo ambayo baraza la madiwa Jiji la Arusha limeyapendekeza ni Soko la Samunge ambalo litapangiliwa vizuri.

Stendi ya daladala Kilombero, kiwanja namba 68 Kilombero, Machame luxury, Uwanja wa ulezi na eneo la Muromboo.

Dkt. Pima amesema maeneo hayo yote Serikali itaweka miundombinu kama vile Vyoo, Maji, Umeme na Barabara ili kuwawezesha wamachinga hao kufanya kazi kwa uhuru.

Nae, mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyabiashara Mkoa wa Arusha bwana  Locken Masawe amesema wanaheshima maelekezo yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kuhusu namna yakuwapanga wamachinga

Aidha, amesema wao kama wafanyabiashara wanapenda kuona Jiji la Arusha linapendeza hivyo wapo tayari kushirikiana na Serikali katika kulifanikisha zoezi hili.

Mwenyekiti wa wamachinga Jiji la Arusha bi. Amina Njoka amesema wao wamefurahishwa na namna Jiji lilivyoyapaendekeza maeneo ya masoko yao kwani hata wao ndio walikuwa wanayaoendekeza hayo.

Kikao hicho ni cha kwanza cha  uzinduzi wa kwanza wa mpango wa kuboresha Jiji la Arusha hususani  namna ya kuwapanga wamachinga katika Jiji la Arusha.





Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa