• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

JIJI LA ARUSHA NDIO SURA YA MKOA WA ARUSHA; WATAKIWA KUJIPANGA KULIPA HADHI YA JIJI LA KIMATAIFA...

Posted on: October 18th, 2023


Na Elinipa Lupembe


Uongozi wa Jiji la Arusha umetakiwa kuweka mkakati thabiti wa kuliweka Jiji hilo kwenye hadhi ya Jiji la Kimataifa kwa kuwa hapo ni kitovu cha utalii na uchumi wa mooa na Taifa la Tanzania.


Rai hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Arusha, Mhe. John V.K. Mongella kwenye kikao kifupi cha maandalizi ya ziara ya siku mbili ya kukagua utekelezaji wa shughuli za maendeleo, kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano Ofisi ya mkuu wa wilaya ya Arusha.  


Mhe. Mongella licha ya kuwapongeza watalamu wa wilaya na Jiji la Arusha kwa kuanza kufanya kazi ya kuliweka Jiji hilo kwenye hadhi kwa kuanza kutekeleza mradi wa kuweka taa za barabarani, amewataka kuweka mpango mkakati wa kulifanya jiji hilo kuwa na hadhi ya Kimataifa.


Amesisitiza kutambua kuwa Jiji la Arusha ndio sura ya mkoa wa Arusha na ndio kitovu cha utalii, asilimia  80%  utalii wa nchi, ni lazima uguse jiji la Arusha hivyo wanayo dhamana kubwa ya kulinda hadhi hiyo na kuifanya itambulike na kila mgeni anayeingia na kutoka Arusha.


 "Mkurugenzi unawajibu wa kuhakikisha jiji linakuwa salama wakati wote, wananchi wanapata huduma stahiki na kuhakikishiwa usalama wao, kwa kuwa eneo hili ni nyeti sana kwa nchi yetu ikiwa ndio kitovu cha utaalii, wekeni taa barabara zote za jiji kwa awamu kadri mapato yanavyopatikana" Ameweka wazi


Aidha amewaelekeza Mkuu wa wilaya, Baraza la Madiwani, Mkurugenzi na watumishi wote, kutumia fursa hiyo adhimu kwa kuwa tofauti kuanzia utendaji kazi, mienendo, mipango na utekelezaji wa kasi, na kuonheza kuwa Jiji la Arusha linatakiwa kuwa mfano kwa halmashauri nyingine kwa kuwa limebeba wajibu mkubwa kama mtoto wa kiume wa kwanza katika mkoa wa Arusha.


"Hakuna asiyefahamu Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amerudisha heshima kubwa kwa Jiji na mkoa wa Arusha, ametupa hadhi ya kuonekana na kutambulika kitaifa na kimataifa, utendaji wake umelifungua Jiji letu,

baada ya Filam ya Tanzania Royo Tour kumetokea mlipuko mkubwa wa watalii ambao umesababisha kuwa na wageni wengi katika Jiji la Arusha na mkoa mzima wa Arusha, Arusha ndio kitovu cha Taasisi na jumuia zake zote za kikanda za Afrika, kwa sasa Taasisi nyingi zimakuja Arusha kwa shughuli mbalimbali pamoja na utalii" Amesema Mhe. Mongella


Ameongeza kuwa serikali ya awamu ya sita imefanya juhudi kubwa za kuifungua nchi, mkoa wa Arusha ukiwa umependelewa zaidi kwa kufungua fursa ambazo zilifungwa kwa kipindi cha nyuma, mikutano mingi ya kitaifa na kimataifa inafanyika Arusha.


Hata hivyo Mhe. Mongella amewapongeza waheshimiwa Madiwani kwa kutekeleza agizo la kuweka taa za barabarani, kwa sasa jiji limepata mwelekeo, kasi hiyo iendelee na kufikia lengo la kwa kutumia wakandarasi wenye bei za soko na kuwataka kuwahimiza wananchi kuchangamkia fursa kupitia wageni wanaoingia Arusha.


Awali mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. John V.K. Mongella amezungumza na uongozi wa wilaya ya Arusha na wakuu wa Idara na vitengo Jiji la Arusha muda mchache kabla ya kuanza ziara ya kukagua shughuli za utekelezaji wa miradi ya maendeleo Jiji la Arusha.


#arushafursalukuki

#KaziInaendelea




Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa