• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

MAMA SAMIA ATOA MKONO WA MWAKA MPYA WATOTO WAISHIO KWENYE MAKAO ARUSHA...,

Posted on: December 30th, 2023



Na Elinipa Lupembe

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa zawadi ya sikukuu za mwaka mpya, maalum kwa ajili ya watoto wanaolelewa kwenye Makao mkoani Arusha.

Akikabidhi zawadi hizo kwa niaba ya Mhe. Rais, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Mongella amesema kuwa zawadi hiyo ya vyakula, imetolewa na Mhe. Rais Samia, maalum kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya mwaka mpya 2024 kwa watoto hao.

Mhe.Rais ametoa zawadi hizo ikiwa ni ishara ya upendo, amani pamoja na moyo wake wa kipekee wa kuwajali watoto wenye mahitaji na waishio kwenye Makao ya kulelea watoto, ili na wao wajisikie kama walivyo watoto wengine wa kitanzania.

"Mhe. Rais amenituma kuleta zawadi hizi kwa niaba yake, kwa kuwa ni kawaida yake, ikifika msimu wa sikukuu hupenda kutoa, zawadi kwa watoto wanaolelewa kwenye Makazi yanayolea watoto wenye uhitaji nchini". ameweka wazi Mhe. Mongella

Aidha amewapongeza walezi wa watoto hao, kwa kazi kubwa wanyoifanya, kazi ambayo ina thamani na thawabu kubwa kwa binadamu na zaidi kwa Mwenyenzi Mungu, kazi ambayo wanaifanya kwa niaba ya Serikali.

Zawadi hii licha ya kuwa ni ishara ya upendo, pia inaonyesha namna Serikali inathamini kazi kubwa inayofanywa na walezi, kazi ambayo ni kuisaidia Serikali katika malezi ya watoto, hususani watoto hawa wenye mahitaji maalumu kutokana na changamoto nyingi zilizowafikisha hapo.

Akizungumza wakati wa kupokea zawasi hizo, Kiongozi wa Makao hayo, Mtawa. Marieta Muyegi, amemshukuru mama Samia na Serikali yake kupitia mkuu wa mkoa wa Arusha, kwa majitoleo ambayo yanaonesha upendo wa hali ya juu kwa watoto waishio kwenye makao.

"Tufikishie salamu zetu kwa Mama Samia, tunatambua mchango wa serikali kwa kuweka mazingira wezeshi ya kuwalea watoto wenye uhitaji nchini, vituo hivi vinafanya kazi kutokana na sera nzuri za Serikali ya awamu ya sita" Ameweka wazi Sista Marietha.

Hata hivyo watoto hao, wameshukuru kwa zawadi hizo, na zenye thamani kubwa kwao na kumuombea kwa Mwenyenzi Mungu amjalie kila lenye kheri katika maisha yake pamoja na uongozi wake.

Naye mtoto, Florentina Philip Mbisha, amemshukuru Mheshimiwa Rais kwa zawadi hiyo na kumuombea kwa Mwenyenzi Mungu amzidishie pale alipotoa na kumzidishia Baraka nyingi katika maisha yake.

Awali, Mhe. Rais ametoa zawadi za chakula na kitoweo yenye thamani ya shilingi milioni 4.3 , kwenye vituo viwili vya makao ya watoto, Makao ya St. Gabriel ya jijini Arusha,  Makao ambayo wanawalea watoto ambao wazazi wao wanatumikia vifungo katika magereza mbalimbali nchini na Makao ya Dhi Nureyn yaliyopo eneo la Ngaramtoni wilaya ya Arumeru.

Zawadi hizo ni pamoja na mchele, sukari, unga wa ngano na sembe, maharage, mafuta ya kula, juisi, boksi za biskuti na mbuzi wawili kwa kila kituo.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa