• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

MHE. MPINA AFUNGUA WIKI YA MAZIWA

Posted on: May 31st, 2018

Waziri wa Mifugo na Uvuvi mheshimiwa Luhanga Mpina, ameiagiza bodi ya maziwa kwa kushirikiana na baraza la kilimo Tanzania kuandaa maonyesho ya kimataifa ya wiki ya maziwa badala kila mwaka kuadhimisha yakitaifa tu.

Ameyasema hayo alipokuwa akufungua maonyesho ya 21 ya wiki ya maziwa kitaifa, yaliyofanyika katika viwanja vya Themi Njiro jijini Arusha.

Amewataka kuendelea kusimamia sheria na kanuna za maziwa zinazotumika katika kila nchi, kwani soko la maziwa linapanuka kwa kasi sana.

Aidha, amesisitiza kuwa serikali inaendelea kuhakikisha inabadilisha sheria na kanuni ambazo zinaonekana hazina tija katika sekta hiyo, hii itasaidia sana katika uboreshaji wa soko la maziwa ndani na nje ya nchi.

Amewahasa wafugaji waendelee kutumia ufugaji wa kisasa kwani utaongeza uzalishaji wa maziwa kwa wingi nakutoa fursa zaidi za masoko kwa nchi za nje.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Arusha ameipongeza sana bodi ya maziwa kwa kufanikisha madhimisho hayo ya wiki ya maziwa na amewataka wazalishaji wazingatie zaidi sheria na kanuni za ndani na nje ya nchi ili kuepuka usumbufu usiokuwa wa lazima.

Magreti Kihumbuli mwakilishi kutoka bodi ya maziwa Kenya, ameishukuru bodi ya maziwa Tanzania kwa kuwapa mwaliko wakushiriki maonyesho hayo.

Amesema anatagemea kujifunza mambo mengi katika maonyesho hayo na hata pia waonyeshaji wa Tanzania watajifunza mengi kutoka kwao na hii itasaidia kuongeza uhusiano bora kati ya nchi hizi.

Luge Kawaga ni mwakilishi kutoka mamlaka ya endelezaji wa maziwa nchini Uganda, amesema maonyesho hayo yatasaidia kubadilisha elimu baina ya nchi hizo tatu.

Maonyesho ya wiki ya maziwa kitaifa yanafanyika mkoani Arusha kwa siku 3 ambapo makapuni takribani 40 yakiwemo ya kigeni yameweza kushiriki maonyesho hayo.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 14, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO YA MIAKA 2 YA MAMA SAMIA AKIWA MADARAKANI

    March 19, 2023
  • BONANZA LA MIAKA MIWILI YA MAMA SAMIA

    March 18, 2023
  • UZINDUZI WA KITABU CHA MIAKA MIWILI YA DKT.SAMIA

    March 14, 2023
  • TUMERIDHISHWA NA MIRADI-KAMATI YA SIASA MKOA

    March 09, 2023
  • Angalia Zote

Video

THE ROYAL TOUR
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa