• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

Mkopo wa bila Riba Watolewa Kwa Akinamama Zaidi ya 600

Posted on: March 24th, 2018

Wanawake wa Arusha watakiwa kutumia vizuri mikopo yao kwa kuwekeza kwenye shughuli  mbalimbali za maendeleo na zitakazo zalisha kwa wingi na kuwaletea mapato yakutosha katika familia zao.

Ameyasema hayo Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na wenye Ulemavu Jenista Muhagama alipokuwa akikabizi hundi ya milioni 120 ya mkopo wa akinamama wajasiliamali, Jiji la Arusha.

Amewataka wanawake waonyeshe kuwa wanaweza kuinuka kiuchumi na kuacha utegemezi huku wakitekeleza majukumu yao katika ngazi za familia na jamii kwa ujumla.

“Mikopo hiyo mnayoenda kupewa ichukulieni kama mmepata tunda la embe katika mti wa miba,yani haitakaa itokee tena mkapatiwa mikopo hiyo kwa mara nyingine”.alisema

Aidha,amewahasa wakatumie vizuri  mikopo hiyo na waache kwenda kununua vitu ambavyo havitawasaidia katika kujiletea maendelea yao na familia zao.

Serikali ya awamu ya tano imelenga katika kuhakikisha matunda ya nchi yanaliwa na kila mtanzania,hivyo fursa hiyo ya wanawake kupatiwa mitaji kwa mikopo isiyo na riba nimkakati mzuri wakutelekeza ilani ya chama cha mapinduzi.

Amesema wizara yake ipo tayari kuwasaidia wakimama wote watakao fanikiwa kumaliza marejesho yao na atawasaidia kupata mikopo mingine ya riba nafuu huku wakiwa katika vikundi.

Pamoja na akimama kipatiwa hiyo mikopo wanaweza pia kutafuta fursa kubwa zaidi katika miradi mikubwa inayofanywa na serikali,ili na wao waweze kukua katika biashara zao.

Amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa juhudi alizozifanya za kusaida makundi maalumu ya vijana,wanawake na wenye ulemevu katika kuwatengenezea ajira zaidi ya 200.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema akinamama ni kundi kubwa sana linalotegemewa kwa asilimia kubwa katika ngazi za familia na jamii kwa ujumla,hivyo aliona hana budi kutafuta namna yakuwawezesha ili waweze kujikwamua katika maisha yao.

Amewataka wenye mapenzi mema waendelee kusaidia akinamama katika Nyanja ya kujikwamua kiuchumi ile pale wanapokosa usaidizi basi waweze kusimama wao kama wao na kuendesha maisha yao na wategemezi wao.

Akisisitiza zaidi Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro,amesema mwanamke nisawa na hewa ya oxjeni pale inapokosekana inaleta maafa makubwa na pengine kupoteza kabisa uhai wa binadamu.

Akitoa salamu za pongezi  Mwenyekiti wa Tanzania Tour Operators (TATO) bwana Wilbad Chambulo kama mmoja wa wadau amesema alichofanya Gambo ni jambo la kuigwa na watu wengine na yeye atachangia kiasi cha milioni 20 ili wakimama wengine 100 waweze kukopeshwa.

Mikopo isiyokuwa na riba ya kuwezesha makundi mbalimbali katika Mkoa wa Arusha ilianza kwa vijana 200 kukopeshwa pikipiki na baada ya kufanya marejesho yao kiasi cha milioni 120 kimetolewa kuwakopesha akinamama 600 kama mtaji wakufanya  biashara mbalimbali.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa