• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

MUUGUZI ASIMAMISHWA KAZI

Posted on: February 8th, 2019

Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania limemsimamisha kazi kwa muda wa mwaka mmoja Muuguzi Msaidizi daraja la kwanza kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mt. Meru Bwana Martini Joseph Chamani kwa kwenda kinyume na maadili ya kazi yake ya uuguzi.

Akisoma hukumu hiyo mwenyekiti wa baraza hilo Bwana Abner Mathube amesema, maamuzi hayo ya baraza yamefikiwa baada ya kusikiliza upande wa mtuhumiwa, mashaidi na mlalamikaji na baraza likaridhishwa na maelezo ya pande zote na kuona kuwa kuna ukiukwaji wa maadili ya kiutendaji kwa muuguzi hiyo.

Abner amesema, Bwana Martini amekutwa na hatia kwa kosa la kuchelewa kuingia kazini na kutumia kilevi wakati wa kazi na kupelekea kushindwa kutimiza majukumu yake ipasavyo.

Aidha, Bwana Abner ametoa rai kwa wauuguzi na wakunga wote nchini kuhakikisha wanafuata maadili ya kazi zao na kuzingatia sheria ili kuepusha migogoro na adhabu kama hizo kutokea mara kwa mara.

Amesema bado mtuhumiwa bwana Martin ana nafasi ya kukata rufaa dhidi ya adhabu hiyo aliyopatiwa na baraza hilo.

Nae Msajili kutoka Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania Bi.Agnes Mtawa anasema kazi kubwa ya baraza ni kuwasajili na kuwasimamia wauguzi na wakunga nchini katika kazi zao, na katika kazi wanaangalia pia nidhamu zao.

Amesema baraza linapoletewa malalamiko juu ya Muuguzi au Mkunga huwa linafuatilia mambo aliyoyafanya na ikithibitika mambo aliyoyafanya ni kinyume na sheria linatoa adhabu, na kwa mujibu wa sheria  ya baraza adhabu zipo za aina tatu; Kumfukuza na kumfuta kwenye dafturi la usajali,kumsimamisha kutoa huduma za uuguzi na ukunga kwa kipindi ambacho baraza litaamua na kutoa kalipio kali.

Kwa shauri hili la Bwana Martin kulingana na taratibu za baraza atatakiwa kurudisha leseni ya uuguzi na vyeti vya usajili na atakapokamilisha adhabu yake atarudishiwa. Anapokuwa nje ya huduma za uuguzi baraza litaendelea kumfuatilia kwa karibu na ikithibitika atafanya matenda kinyume na taratibu ikiwemo kutoa huduma za uuguzi na ukunga wakati amesimamishwa kazi atafutiwa kabisa usajili wake.

Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania limefanya kikao chake cha 196 Mkoani Arusha na moja ya agenda ilikuwa kusikiliza mashitaka dhidi ya muuguzi Bwana Martin kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mt.Meru.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa