• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

Mwanaume jali afya yako,Pima

Posted on: August 29th, 2018

Watakaogundulika wana maambukizi ya virusi vya UKIMWI wanatakiwa kuwaleta wenza wao wapimwe  pia ili waweze kujitambua na kuishi mda mrefu.

Ameyasema hayo Mkuu wa Wilaya ya Monduli  Idd Kimanta kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo katika uzinduzi wa kampeni ya upimaji wa virusi vya UKIMWI kwa hiari ijulikanayo kama “FURA YANGU”.

Gambo amesema bado idadi ya wanaume wanaoenda kupima ni ndogo sana ukilinganisha na wanawake, hivyo nguvu za uhamasishaji inaitajika zaidi kwa wanaume.

Ikiwezekana hata kutumia mikusanyika kama sehemu za ibada na maeneo ya starehe ili kuweza kuwapata wanaume wengi na kuwahamasisha wajitokeze zaidi.

Pia wataalamu wanatakiwa kuongeza zaidi wigo wa utoaji huduma hii kama kutoa ushauri nasaha na kuwahamasisha wagonjwa wapime kwa hiari.

Akitoa takwimu za hali ya maambukizi kwa mkoa wa Arusha Mganga mkuu wa mkoa Vivian Wonanji, amesema kwa mwaka 2011/2012 hali ya maambukizi imeshuka sana kutoka 3.2% hadi 1.9 kwa mwaka 2017/2018.

Amesema hali hii ni nzuri sana kwa mkoa wetu lakini hatutakiwi kupunguza nguvu hii ya upimaji wa hiari na matumizi ya dawa kwa wagonjwa kwani mpaka sasa waliogundulika na VVU ni 52.2% wenye umri kati ya miaka 15-64 ambapo wanaume ni 45.3%na wanawake ni 55.9%.

Hali hii inaonesha kuwa bado jitihada inaitajika kuhamasisha wanaume wajitokeze zaidi katika upimaji na sio upimaji tu hata pia matumizi ya dawa kwani kati ya wagonjwa 90.9% wanaotumia dawa wanaume ni 86.2% tu na wanawake ni 92.9%.

Aidha, amesisitiza zaidi hata katika hatua ya kufubaisha VVU kwa wagonjwa wanaotumia dawa bado msukumo ni mdogo kwa wanaume kwa 84% kati ya wagonjwa 87.7%.

Kupitia kampeni hii ya Furaha yangu yenye ujumbe wa Pima,Jitambue,Ishi itasaidia zaidi kuwahamasisha wanaume kupima kwa hiari.

Akitoa takwimu za upimaji katika kampeni hii kuanzia Agosti 17, 2018 wilayani Monduli mwakilishi kutoka Mkapa Foundation David Mnkhally amesema,jumla ya watu 5,730 ndio wameweza kupima na 29 ndio wamegundulika na maambukizi ya VVU.

Ikiwa katika kata ya Monduli Juu jumla ya watu 2.987 wamepima na kati yao wanaume ni 1,206 sawa na 40.3% na wanawake ni 1,781 sawa na 59.6% na kata ya Meserani waliopima ni 2.743,wanaume ni 1,378 sawa na 50.2% na wanawake ni 1,365 sawa na 49.7%.

Kampeni hii ya Furaha Yangu ilizinduliwa rasmi mnamo Juni 2018 na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa jijini Dodoma, na kwa mkoa wa Arusha zimezinduliwa rasmi Agosti 28, 2018 katika kata ya Meserani wilayani Monduli na itaendelea katika wilaya ya Ngorongoro.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa