• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

Rais Magufuli Azindua Kituo cha Polisi cha Utalii

Posted on: April 7th, 2018

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, ametoa Bilioni 10 kwa ajiri ya ujenzi wa nyumba za polisi wa vyeo vya chini nchi nzima.

Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na jeshi la polisi la mkoa wa Arusha katika sherehe za kuzindua  ofisi ya kidiplomasia ya utalii,Nyumba za makazi ya polisi na vituo 2 vya polisi wilayani Arusha.

Amesema kutokana na juhudi zilizofanywa na mkoa wa Arusha wa kujenga nyumba za polisi 31 baada ya nyumba 13 kuungua na moto mnamo Septemba 2017 na kusababisha familia 14 kukosa makazi.

Amewataka wakuu wa Mikoa wengine nchini kuiga mfano huo wa kujenga nyumba za polisi kwa  kuwashirikisha wadau mbalimbali kwani zilizoungua ni 13 na zimejengwa 31 zaidi ya zilizoungua.

Hata hivyo amewashauri pia wabunge watumie kiasi cha fedha cha mfuko wa jimbo katika kusaidia kujenga nyumba za polisi katika majimbo yao badala ya kuwaachia wakuu wa mikoa peke yao.

Aidha, Magufuli ametoa ajira 1500 ya wahitimu wa jeshi la kujenga Taifa(JKT) kuajiriwa katika jeshi la polisi, ili kuongeza nguvu zaidi katika maeneo mbalimbali ya nchi katika kulinda usalama.

Amelitaka jeshi la polisi kuendelea kuchapa kazi kwa bidii kwani amefurahishwa na maonyesha yaliyoonyeshwa katika sherehe hizo ambayo yametoa picha nzuri kwa nchi kuwa jeshi la polisi lipo imara na yeye ataendelea kuwaunga mkono kwa kila watachoamua kufanya.

Magufuri amelitaka jeshi la polisi nchini kurekebisha mapungufu madogo madogo yaliyojitokeza katika jesho hilo yakiwepo ya rushwa na uonevu kwa wananchi ambayo yamekuwa yakichafua jina la jesho hilo kwani yanafanywa na baadhi ya polisi.

Akisoma taarifa fupi ya ujenzi Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Simon Sirro amesema ujenzi wa kituo cha polisi cha kidiplomasi kimegharimu kiasi cha shilingi milioni 193 ambapo ni michango kutoka kwa wadau na serikali.

Aidha, katika ujenzi wa kituo cha polisi cha Murieti kimegharimu kiasi cha milioni 260 na ujenzi wa nyumba za polisi 31 zimegharimu kiasi cha milioni 550 ambapo milioni 250 zimetoka serikalini,milioni 50 zimetolewa na polisi na wadau mbalimbali wamechangia kiasi cha milioni 250.

Amesema jeshi la polisi nchini limeendelea kulinda usalama wa raia na mali zao na hivyo kupelekea kupunguza matukio ya uharifu kwa kiasi kikubwa na hata pia kudhibiti ajari za barabara kwa kiwango kikubwa.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amemshukuru Rais kwa juhudi zake alizozifanya katika kuleta maendeleo kwa mkoa wa Arusha katika nyanja mbalimbali hasa upatikanaji wa maji safi, ujenzi wa barabara,uboreshaji wa huduma za afya na kuboresha elimu kwa ujumla.

Aidha, amesema mkoa wa Arusha umeendelea kuleta maboresho zaidi katika sekta ya elimu kwa kuandaa utaratibu wa kutunga mtihani mmoja kwa shule zote za mkoa wa Arusha,ambapo awali kila shule ilikuwa inaanda mitihani yake.

Rais Magufuli yupo mkoani Arusha kwa ziara ya kikazi ya siku 2 ambapo alitokea mkoani Manyara huko  alikabidhiwa ukuta wa machimbo ya Mirerani na sasa anaendelea na ziara  yake mkoani Arusha.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa