• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RAS ARUSHA ATETA NA WATUMISHI ARUSHA DC; AWATAKA KUFANYAKAZI KWA WELEDI NA UADILIFU....

Posted on: October 9th, 2023

Na Elinipa Lupembe


Katibu Tawala mkoa wa Arusha Massaile Albano Musa amewata watumishi kufanyakazi kwa weledi na uadilifu kwa kuzingatia kanuni sheria na taratibu za utumishi wa Umma na kuachana na vitendo viovu ambavyo ni kinyume na maadili ya taratibu za kazi .


Katibu Tawala amesema hayo wakati wa kikao kazi, kilichowakutanisha watumishi wa sekta zote chenye lengo la kusikiliza kero za watumishi sambamba na kuwambushana utekelezaji bora wa majukumu ya kazi katika kuwatumikia wananchi.


Amewasisitiza watumishi kuwa, wanalo jukumu kubwa la kuwahudumia wanachi kwa niaba ya serikali hivyo wanapaswa kufanya kazi kwa uadilifu,  kuwa na nidhamu katika kazi pamoja na kutunza siri za serikali kwa kufuata maelekezo ya viongozi kwa kuzingatia kanununi, sheria, miongozo na taratibu za utumishi wa Umma.


"Fanyenyeni kazi kwa  upendo, shirikianeni, heshimianeni kwa  kutambua umuhimu wa kila mtu kwa nafasi yake ili kufikia malengo ya serikali ya awamu ya sita ya kuwahudumia wananchi, serikali imewaamini, rudisheni fadhila kwa wananchi" Amesema Katibu Tawala huyo


Aidha ameutaka uongozi wa halmashauri kuimarisha mahusiano bora kazini kwa kusimamia stahiki na maslahi ya watumishi ikiwemo malipo ya likizo, stahiki za ugonjwa,  wastaafu pamoja na malipo ya uhamisho bila kujali nani ni nani.


"Idara ya utawala simamieni Maafisa Watendaji wa kata na vijiji kuhakikisha wanafanya vikao na mikutano ya kisheria ngazi za vijiji na kata, kwa kila robo ya mwaka na kuwasilisha mihtasari ya vikao na mikutano ofisi ya mkurugenzi" Amesema


Pia amewataka Maafisa Elimu kata kusimamia vema sekta ya elimu katika shule, licha ya kusimamia taaluma shuleni zaidi kusimamia ulinzi na usalama wa mtoto kuanzia nyumbani mpaka shuleni, upatikanaji wa chakula cha mchana kwa wanfunzi.


Hata hivyo watumishi wa halmashauri ya Arusha wamemshukuru Katibu Tawala kwa kufanya kikao pamoja nao, kikao ambao licha ya kutoa kero zao kimewakumbusha majukumu yao ya kazi na kuahidi kufanyia kazi maelekezo yaliyotolewa ili kufikia lengo la serikali la kuwahudumia wananchi.


Afisa Tarafa ya Mukulat Tatu Furaisha, amemshukuru RAS kwa kikao kazi hicho na kubainisha kuwa kiongozi anapokutana na watumishi ni afya katika kazi na kuahidi kufanyia kazi malekezo yote ikiwemo nidhamu ya kazi.


Naye Katibu Tawala Arumeru Joseph Mabiti, ameahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa hususani katika kata na vijiji kwa kuhakikisha vikao na mikutano ya kisheria inafanyika kwa wakati  ili kuongeza uwazi wa shughuli za serikali kwa maendeleo ya wananchi.


Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, amethibistisha kupokea maelekezo na kuendelea kuwasimamia watumishi kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Kanuni, Sheria na taratibu huku akiahidi kuendela kutoa stahiki za watumishi kwa kuzingatia taratibu za utumishi wa Umma.


ARUSHA FURSA LUKUKI

#KaziInaendelea



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa