• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MAKKALLA : KITUO CHA NAMANGA KIKUZE BIASHARA YA TANZANIA NA KENYA..

Posted on: September 4th, 2025

 __Ameahidi kushughulikia upatikanaji wa Skana kituoni hapo__

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla @amosmakalla leo Alhamisi Septemba 04, 2025 ametembelea na kukagua utoaji wa huduma kwenye Kituo cha forodha cha Pamoja kwenye Mpaka wa Namanga Mkoani Arusha, akiwataka watumishi wa Taasisi zote 18 za serikali zinazotoa huduma kwenye kituo hicho kuongeza ufanisi katika utendaji ili kukuza biashara kati ya Mataifa ya Tanzania na Kenya.

Aidha Mhe. Makalla akizungumza na Watumishi wa Taasisi hizo ameahidi kushirikiana na Waziri wa fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba @mwigulunchemba na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Yusuph Juma Mwenda @tratanzania kuhakikisha inapatikana Skana ya ukaguzi wa mizigo kwenye kituo hicho cha forodha ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wageni na watanzania wanaotumia mpaka huo kuingia nchini.

"Skana kwa Tanzania ipatikane haraka, haiwezekani kwa mapato haya tukose Skana,  tupate skana turahisishe biashara na ile adhma ya kurahisisha biashara tuione kwa vitendo ili sisi tusiwe kikwazo, nitalisukuma hili kwa nguvu zote na skana tuipate kwa uharaka." Amesema Mhe. Makalla wakati akizungumza na watumishi kutoka Taasisi 18 za serikali zinazofanya kazi kwenye kituo cha Namanga.

Katika maelezo yake, Mhe. Makalla pia amewakumbusha watumishi hao kuwa wamebeba dhamana na taswira ya nchi katika kutoa huduma kwa wageni na watalii wanaoingia nchini kwa kupitia mpaka wa Namanga akiwahimiza pia kufanya kazi kwa bidii katika kutimiza malengo na maono ya Viongozi wa pande mbili, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan @samia_suluhu_hassan na Rais Dkt. William Ruto wa Kenya.

Awali wakati akimkaribisha kwenye Kituo hicho cha Namanga, Mkuu wa Wilaya ya Longido Mhe. Salum Kalli amemueleza Mhe. Makalla kuwa kupatikana kwa Skana hiyo kutarahisisha zaidi biashara na muingiliano wa watu kupitia mpaka huo pamoja na kupunguza muda mrefu unaotumika kwenye ukaguzi wa magari ya mizigo yanayoingia nchini kupitia mpaka huo unaotumika kwenda Kenya, Uganda, Sudani Kusini na Somalia.

@maelezonews @urtmof @tratanzania @ppra_tanzania @monduli_dc @longido.di

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO MTIHANI WA UTAMIRIFU (MOCK) 2025 DARASA LA SABA (VII)- MKOA WA ARUSHA June 07, 2025
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKALLA AUNDA TUME KUFUATILIA SAKATA LA MACHINJIO NGORBOB ARUMERU..

    September 09, 2025
  • WAMAREKANI WATALII KWA WINGI TANZANIA- KAIMU BALOZI MAREKANI TANZANIA..

    September 11, 2025
  • RAIS SAMIA KUZIUNGANISHA MONDULI NA NGORONGORO KWA BARABARA YA LAMI..

    September 10, 2025
  • KILA LA KHERI DARASA LA SABA 2025..

    September 10, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa