• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MAKONDA AAHIDI KUTEKELEZA AHADI ZAKE ZOTE...

Posted on: May 17th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda ameahidi kuwa ndani ya siku mia moja za uongozi wake Mkoani Arusha atakuwa amekamilisha ahadi zake zote alizoziahidi tangu alipoteuliwa Machi 30, 2024 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Mhe. Mkuu wa Mkoa Paul Christian Makonda ametoa kauli hiyo leo Mei 16 wakati alipokuwa akikabidhiwa pikipiki 20 kwaajili ya kuimarisha Ulinzi na usalama Mkoani Arusha, pikipiki ambazo zimetolewa na Benki ya Biashara ya CRDB ikiwa ni sehemu ya programu yake ya kurudisha kwenye Jamii.


Mhe. Mkuu wa Mkoa amesema miongoni mwa ahadi zake ilikuwa ni pamoja na kuliimarisha Jeshi la Polisi kwa kuwapatia Nyenzo za ufanyaji wa kazi katika kuimarisha Ulinzi na usalama Mkoani Arusha ambapo aliahidi kuwatafutia pikipiki 50, Baiskeli za Umeme 100 na magari 20 kutoka kwa wadau mbalimbali wa Maendeleo.


Mhe. Makonda amesema anatambua kuwa Usalama ni kivutio namba moja katika kuvutia utalii Mkoani Arusha na hivyo ameishukuru Benki ya CRDB kwa kumuunga mkono Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika maagizo yake kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha ya kuhakikisha anakuza utalii kwenye mkoa wa Arusha.


Mhe. Mkuu wa mkoa pia amewakaribisha wawekezaji na wafanyabiashara mbalimbali kuendelea kuwekeza Mkoani Arusha na anasema kufikia Mwezi Julai tarehe 30 Biashara ndani ya Mkoa wa Arusha zitakuwa zinafanyika kwa saa 24 kwani Usalama na Ulinzi wa mkoa utakuwa umeimarika kwa kiwango cha juu kabisa.


Katika hatua nyingine Mhe. Mkuu wa Mkoa amemuomba Mkurugenzi Mtendaji Benki ya CRDB, Bw. Abdulmajid Nsekela kuandaa Mpango maalumu wa usaidizi wa mikopo kwa wawekezaji wa ndani, ili kuwezesha Ujenzi wa Malazi ya kutosha Mkoani Arusha katika jitihada za kuondoa ufinyu wa nyumba za kulala wageni na watalii wanaofika mkoani Arusha kutalii na kwenye mikutano na warsha mbalimbali.


Mhe. Mkuu wa Mkoa pia amevishukuru vyombo vya ulinzi na usalama Mkoani Arusha kwa kuendelea kupunguza uhalifu kwa kasi kubwa akihaidi kuendelea kushirikiana nao katika kuwawezesha vitendea kazi na dhana mbalimbali ili kuondosha vikwazo katika majukumu yao.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa