• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MAKONDA AMUAGIZA DC ARUSHA KUTENGA BARABARA ZA JIJI KWA AJILI YA MAONESHO YA WAJASIRIAMALI

Posted on: April 28th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh. Paul Christian Makonda amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Arusha kutenga barabara maalumu katikati ya jiji, itumike kwaajili ya Maonesho ya kibiashara kwa wajasiriamali wa mavazi ya asili, Picha, Vinyago na bidhaa nyingine za Urembo kuelekea kwenye kilele cha siku ya wafanyakazi duniani.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amemuagiza Mkuu wa Wilaya Mh. Felician Gasper Mtahengerwa kuwa barabara hiyo iwe pembezoni mwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, uwanja uliotengwa kwaajili ya kutumika kwenye sherehe za Mei Mosi, akitaka ianze kutumika Jumatatu ya wiki ijayo.

Mkuu wa Mkoa Ametoa kauli hiyo leo Aprili 27,2024 wakati kikao kazi na viongozi wa Chama cha Wafanyakazi na kamati mbalimbali za maandalizi ya sherehe za wafanyakazi ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mh. Makonda amesema wananchi wa Mkoa wa Arusha wanapaswa kunufaika na shughuli mbalimbali za kitaifa zinazofanyika Mkoani hapa na hivyo kuwataka wananchi kujiandaa kutumia fursa zinazotokana na ugeni ambao tayari umeshaanza kuwasili Jijini Arusha kujiandaa na sherehe hizo.

Katika hatua nyingine Mh. Mkuu wa mkoa amewahakikishia usalama wa kutosha wakazi wa Arusha na wageni wote wanaofika mkoani Arusha kwenye shamra shamra za kuelekea kwenye Kilele cha siku ya wafanyakazi duniani.

Mheshimiwa Mkuu wa mkoa ametumia fursa hiyo pia kuwaomba wananchi wa Arusha na mikoa jirani kujitokeza kwa wingi katika sherehe hizo za Mei Mosi kama sehemu ya kuwaenzi na kuenzi kazi nzuri zinazofanywa na watumishi na wafanyakazi mbalimbali.

Katika Kikao hicho Mkuu wa mkoa pia ametangaza kuanza kwa shamra shamra za kuelekea siku ya wafanyakazi ikiwemo michezo ya sarakasi na vikundi mbalimbali vya sanaa ambavyo vitakuwa vikizunguka maeneo mbalimbali ya Jiji la Arusha.

Kwa Upande wake Rais wa Vyama vya wafanyakazi TUCTA Bw.Tumaini Nyamhokya amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa ubunifu wake kwenye kukoleza shamra shamra za Mei Mosi mwaka huu akiutaja ujana wake kama silaha muhimu iliyoongeza mambo mengi mapya kwenye sherehe za mwaka huu jijini Arusha.

Nyamhokya ametumia fursa hiyo pia kutangaza kuhusu mbio za marathoni zitakazozinduliwa kesho jumapili Aprili 28, 202

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa