• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MAKONDA AMUOMBA RAIS MWINYI KUIUNGANISHA ARUSHA NA ZANZIBAR KUKUZA UTALII....

Posted on: May 18th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amemuomba Mhe.Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi kuiunganisha Zanzibar na Mkoa wa Arusha kwenye sekta ya utalii ili kuwezesha mabadilishano ya Watalii wa pande hizo mbili.


Mhe. Makonda pia amemuomba Mhe. Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi kutangaza fursa na vivutio vya Uwekezaji vilivyo Mkoani Arusha katika adhma ya kutimiza maelekezo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuongeza vyumba na Vitanda vya kulala wageni mkoani Arusha.


Mkuu wa Mkoa wa Arusha ametoa maombi hayo mbele ya Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi ambaye leo ndiye mgeni rasmi kwenye Semina maalum ya wanahisa wa Benki ya CRDB, semina inayofanyika kwenye Kituo cha kimataifa cha Mikutano mjini Arusha - AICC.


Katika hatua nyingine Mhe. Mkuu wa mkoa ameishukuru benki ya CRDB kwa kuwa mdau mkubwa wq maendeleo ya Mkoa wa Arusha pamoja na kuichagua Arusha kuwa Mwenyeji wa semina ya wanahisa na Mkutano Mkuu wa 29 wa wanahisa unaotarajiwa kufanyika Mei 18, 2024 Jijini Arusha.


Katika majibu yake Mhe. Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi amemuahidi Mhe. Mkuu wa Mkoa kuwa atatetekeleza maombi yake ipasavyo hasa katika suala la uwekezaji wa ujenzi wa hoteli na nyumba za kulala wageni kutokana na idadi kubwa ya Wawekezaji wanaofika Zanzibar kutaka kuwekeza kwenye ujenzi wa nyumba na vyumba vya kulala wageni na watalii wanaofika nchini.


Akiapishwa mwishoni mwa Mwezi Machi Mwaka Huu, Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan alimuagiza Mkuu wa mkoa wa Arusha kupambana katika kukuza utalii wa Arusha pamoja na kuongeza idadi ya vyumba na vitanda vya kulala wageni na watalii kutokana na upungufu mkubwa unaokadiriwa kutokea kutokana na matokeo chanya ya filamu ya The Royal Tour iliyokuwa na nia ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini Tanzania ikiwemo vile vilivyopo mkoani Arusha.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa