Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda, ameungana na waumini wa Kanisa la Kiinjili la kiluther Tanzania pamoja na washiriki wengine katika mbio zilizolenga kusaidia elimu jumuishi na huduma ya shufaa kwa watoto walioko katika mazingira magumu.
Mbio hizo zimefanyika leo 21 Juni, 2025 katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha ambapo Mhe. Makonda amesisitiza suala la kulinda amani na kushauri Kanisa kufuata misingi yake badala ya kugeukia Ulimwengu.
Mbio hizo zimeambatana na kaulimbiu isemayo " kimbia kwa moyo, saidia kwa upendo".
Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa