• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA AAGIZA KUONGEZA KASI YA UJENZI WA BWENI JIPYA LA WAVULANA SEKONDARI KITUMBEINI

Posted on: January 31st, 2024


Na Elinipa Lupembe


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John V.K Mongella amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa bweni la wavulana shule ya Sekondari Kitumbeini, kijiji cha Lopolosek, wilaya ya Longido na kuwasisitiza kuongeza kasi iya ujenzi ili likamilike na kuanza kutumika.


Mhe. Mongella amemuagiza Mkuu wa wilaya hiyo, kusimamia mafundi usiku na mchana ili waongeze kasi ya ujenzi na liweze kukamilika, ili lianze kutumiwa na wanafunzi hao, wenye uhitaji mkubwa, kulingana na idadi kubwa ya wanafunzi shuleni hapo.


Mradi huo wa bweni unatakelezwa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF, OPEC awamu ya IV, kwa gharama ya shilingi milioni 155.4, bweni ambalo linategemea kukamilika mwishoni mwa mwezi Februari, 2024.


Mkuu wa shule hiyo, Mwl. ameweka wazi kuwa, lengo la ujenzi wa bweni hilo ni kuwezesha upatikanaji wa malazi bora kwa wanafunzi ili kurahisisha tendo la kujifunza na kufundisha kwa walimu na wanafunzi hasa kwa kuzingatia mazingira rafiki kwa wanafunzi hupandisha taaluma na kuongeza kasi ya ufaulu.


Hata hivyo wananchi wa Kijiji cha Lopolosek ilipo shule hiyo, wameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuona umuhimu wa kujenga bweni hilo la wavulana, litakalosaidia watoto wao kupata elimu bora,  kwa kulala shuleni tofauti na wanapolala nyumbani, ambapo hulazimika kutembea umbali mrefu kwenda na kurudi shuleni. 


Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Msimamizi wa mradi huo, gazi ya jamii, Isaya Laizer, amesema kuwa, kutokana na mazingira hatarishi ya eneo hilo wanafunzi wote hulazimikq kulala shuleni, hivyo bweni hilo ni muhimu kwa watoto hao, kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaopangiwa shuleni hapo na kusababisha shule kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi kila mwaka.


"Tunamshukuru rais wetu, mama Samia kwa kazi nzuri anayoifanya, tunamuombea afya njema ili aendelee kuwatumikia watanzania, kwa kipindi kifupi amefanya kazi kubwa inauoonekana, Kitumbeini ni mbali mwisho wa dunia, tulisahaulika kwa miaka mingi lakini awamu hii ya sita, kila pesa zinakuja kila kona ni maendeleo ya Mama Samia" Amebainisha Leskari Loserian Laizer



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa