• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA AKEMEA TABIA YA KUONGEZA FEDHA ZA MIRADI KUTOKA MAPATO YA NDANI....

Posted on: November 8th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. John V.K. Mongella,  amekemea tabia ya wahandisi kuletewa fedha za miradi kutoka Serikali Kuu na kutokukamilisha mradi kwa fedha hizo na baadaye kupanga kuongeza fedha kutoka mapato ya ndani.

Amesema hayo mara baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari ya kata Mundarara wilaya ya Longido na kupewa tarifa ya fedha zilizotolewa na serikali milioni 470, haziweza kukamilisha mradi huo na kupanga kuongeza fedha kutoka mapato ya ndani.

Mhe. Mongella licha ya kuuagiza uongozi wa wilaya ya Longido kukamilisha ujenzi wa mradi huo kwa maeneo madogo yaliyosalia ifikapo Desemba 15, mradi ukuwa umezingatia vigezo vya ubora vilivyoainishwa na Serikali, na kuwasisitiza kuhakikisha fedha zilizotolewa na Serikali Kuu, zinakamilisha mradi huo bila kuongeza fedha kutoka mapato ya ndani.

Aidha amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mhe. Marco Ng'umbi kuwasimamia watendaji wote wa chini yake, kusimamia utekelezaji wa miradi yote ya maendeleo na kuhakikisha inakamilika kwa wakati na kwa fedha zilizoletwa na Serikali na si vinginevyo kwa kuwa fedha zote zinakuja zikiwa na maelekezo yake.

"Fedha za Mapato ya ndani tayari zina mpango wa bajeti ya matumizi yake, mnapoingiza matumizi
 mengine nje ya bajeti mnasababisha kuua kazi zilizopangwa na kusafanya shughuli na mipango ya halmashauri kupitia mapato ya ndani kukwama na kushindwa kufikia malengo" Amesema Mhe. Mongella

Aidha amewataka watendaji wote wa Serikali na viongozi wa wananchi, Baraza la Madiwani na  Kamati ya fedha, kubadilika katika usimamizi wa miradi, serikali imewapa dhamani ya kusimamia shughuli za serikali ili wananchi waweze kupata huduma za kijamii kisekta kama yalivyo malengo ya Serikali.

"Tuweni wazalendo kwa kuwahurumia na kuwasaidia watoto wetu, watoto wa kitanzania hawana hatia, kwa kusimamia vizuri utekelezaji wa miradi hii ya  elimu, watoto wetu wanakwenda  kunufaika nayo" Ameweka wazi Mhe. Mongella

Awali Serikali kupitia programu ya Kuboresha Miundombinu ya Shule za Sekondari Nchini (SEQUIP), imetoa shilingi milioni 470 za kujenga shule mpya ya sekondari ya kata ya Mundarara, fedha zinazotumika kujenga vyumba 8 vya madarasa, jengo la Utawala, majengo ya maabara, maktaba, chumba cha TEHAMA, matundu 16 ya vyoo pamoja na tanki kubwa la kuhifadhia maji lenye kujazwa lita elfu 10


#ArushaFursaLukuki

#KaziInaendelea



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa