• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA AMALIZA MGOGORO WA MPAKA KATI YA KIJIJI CHA BUGER NA HIFADHI YA TAIFA YA ZIWA MANYARA....

Posted on: December 29th, 2023

Na Elinipa Lupembe.


Mgogoro wa muda mrefu wa mpaka baina ya Kijiji cha Buger na Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, uliodumu zaidi ya miaka 15, hatimaye umetatuliwa na ufumbuzi wake kutangazwa rasmi na Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mhe. John V.K.Mongella.


Mhe. Mongella ametangaza utatuzi wa mgogoro huo, mara baada ya kazi aliyoiagiza kamati ndogo iliyoundwa ikijumuisha watalamu na wawakilishi wa kijiji cha Bugeli, kukamilika na kupata suluhisho la kudumu, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Buger.


Mhe. Mongella amesema kuwa, kamati imekuja na maamuzi ambayo yanagusa pande zote mbili, ambapo kila upande umeathirika kwa kumegwa eneo, huku eneo la hifadhi za Eka 8.3, wakiwachiwa wananchi pamoja na eneo lililojengwa nyumba tatu za wananchi, likiachiwa wananchi hao kuendelee kumiliki.


Amewasisitiza wananchi hao sasa kuachana na mgogoro na kujikita kufanya kazi za uzalishaji mali, shughuli ambazo zitaleta maendeleo ya familia na taifa kwa ujumla wake na kuweka wazi kuwa eneo la kijiji na eneo la hifadhi yote ni mali ya Umma na kila mwananchi anayodhamana ya kuilinda ardhi hiyo.


"Kila mwananchi anawajibu wa kulinda eneo la hifadhi kwa kutambua thamani yake, ambayo wananchi wa Bugali wananufaika nayo, mnapata unyevuunyevu ambao unawawezesha kufanya kilimo cha mwaka mzima, hii ni kutokana na uwepo wa eneo la uhifadhi linalotunzwa, hivyo ni wajibu wetu kuendelea kutunza eneo hili kwa manufaa yetu na vizazi vijavyo" Ameweka wazi Mhe. Mongella.


Aidha, ameuagiza uongozi wa Hifadhi hiyo, kuanza kuweka alama za mipaka 'bicon', kwa kuzingatia vipimo vya mipaka iliyokubalika na baada ya alama hizo kuweka barabata za kupitika ili wananchi watambue mipaka yao, ambayo itakuwa wazi kwa kila mtu.


Akisoma maamuzi ya Kamati, Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi - ACC Eva Mallya, amesema kuwa mpaka huo umezingatia pande zote mbili ambapo takribani Eka 8.3 za hifadhi ambapo nyumba tatu za wananchi pamoja ja kisima cha maji zilizongia eneo la hifadhi limeachiwa wananchi huku baadhi ya vipande vya ardhi, ambavyo walikuwa wakilimwa vikirudi eneo la Hifadhi.


Naye Afisa Ardhi mkoa wa Arusha, Daniel Mruma, ameweka wazi kuwa, Idara ya ardhi imeshirikiana na timu iliyoundwa na Mkuu wa mkoa wa Arusha na pande zote mbili kufikia muafaka wa eneo la hifadhi kuachia Eka 8.3 na kazi inayofuata ni kuweka alama mpya za mipaka kwenye maeneo hayo.


Awali, mwezi uliopita Mkuu wa mkoa wa Arusha, alikutana na wananchi wa Buger na kujadili mgogoro huo na kuunda kamati ya makubaliano ambayo imekuja na maamuzi ambayo ndio suluhisho la kudumu la mgogoro huo.



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa