• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA AMEWATAKA WANANCHI KUJITOKEZA KUCHANGIA DAMU

Posted on: January 21st, 2024

Na Daniel Gitaro

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John V.K Mongella amewataka wananchi wa mkoa huo, kujitokeza katika zoezi la Kitaifa la Kuchangia Damu Salama, na kujitolea damu ili kuokoa maisha ya watu wanaohitajia damu kwa dharura.


Mhe. Mongella ametoa wito huo wakati wa uzinduzi wa zoezi la Uchangiaji Damu Kitaifa liliandaliwa na Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania na kuwakutanisha wadau kutoka madhehebu yote nchini, zoezi liliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Mkoa wa Arusha.


Amesema kuwa, zoezi hilo linalenga kukusanya damu Salama na ili kuwa na akiba ya damu kwenye hospitali zetu, damu ambayo itatumika kwa wagonjwa wenye uhitaji, hususani wagonjwa wa dharura waliopata ajali na kuokoa maisha, ikiwa ni kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya maridhiano inayotarajiwa kufanyika Machi 6, 2024.


Kujitolea damu ni tendo la thawabu kubwa kwa Mungu,  kwa kuwa damu ni zao pekee ambalo haliwezi kununuliwa kwa thamani yoyote ya fedha, bali kwa kujitolea kwa wananchi wenyewe.


“Ninawaomba wanaarusha tujitokeze kwa wingi kuchangi damu,kwa kuwa kuna uhitaji mkubwa sana wa damu salama, Damu ni uhai hivyo unapotoa sehemu ya uhai wako na kuokoa wengine unapata thawabu kutoka kwa Mwenyenzi Mungu"


Hata hivyo, amethibitisha kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea na mkakati wa kuboresha miundombinu ya sekta ya afya na vifaa tiba, lakini yote hayo yatakuwa na manufaa zaidi ikiwa wananchi watajitoa kwa wingi kuchangia Damu Salama.


Naye Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Sheikh, Dkt. Alhad Mussa Salim, licha ya kuendelea kusisitiza wananchi kushiriki katika zoezi hilo, ameipongeza Serikali ya Awamu ya sita kwa kuendelea kudumisha amani nchini, katika masuala ya kidini na kisiasa jambo ambalo linaleta umoja kwa wananchi wake.


“Sisi tunafanya maridhiano na amani katika nchi yetu, lakini wananchi hawawezi kuwa na amani kama wanasumbuliwa na maradhi na zoezi hili la kuchangia damu halibagui dini wala imani yoyote bali hii ni kama sadaka na ibada yenye maana Zaidi.”


Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Taifa, Askofu Israel Maasa amemshukuru sana Mkuu huyo wa Mkoa kama mlezi wa Jumuiya hiyo Mkoani hapo kwa ushirikiano mkubwa anaoonyesha katika kuleta maridhiano ka kuhakikisha kuwa Amani inadumu.


Hata hivyo, ameongeza kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea na mkakati wa kuboresha miundombinu ya sekta ya afya, ununuzi wa vifaa na vifaa tiba hasa katika mkoa wa Arusha lakini yote hayo yatakuwa na manufaa Zaidi ikiwa wananchi watajitolea michango yao ikiwemo kuchangia damu salama kwa wahitaji.


Naye Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Sheikh, Dkt. Alhad Mussa Salim, licha ya kuendelea kusisitiza wananchi kushiriki katika zoezi hilo la Kitaifa ameipongeza Serikali ya Awamu ya sita kwa kuendelea kudumisha Amani katika Nchi yetu katika masuala yote ya kidini na kisiasa jambo ambalo linaleta umoja kwa wananchi wake.


“Sisi tunafanya maridhiano na Amani katika nchi yetu, lakini wananchi hawawezi kuwa na Amani kama wanasumbuliwa na maradhi na zoezi hili la kuchangia damu halibagui dini wala Imani yoyote bali hii ni kama sadaka na ibada yenye maana Zaidi.”


Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Taifa, Askofu Israel Maasa amemshukuru sana Mkuu huyo wa Mkoa kama mlezi wa Jumuiya hiyo Mkoani hapo kwa ushirikiano mkubwa anaoonyesha katika kuleta maridhiano ka kuhakikisha kuwa Amani inadumu kwenye Mkoa huo.


Ameongeza kuwa, Jumuiya hiyo imeridhia kuingia ubia na Serikali kuhakikisha kuwa masuala yote yahayohusiana na Amani yanaendana pia na maendeleo ya kijamii ambayo yanaambatana na wananchi kuwa na afya njema.


“Tunaamini hatuwezi kuridhiana katika masuala ya kuabudu kwasababu kila mtu ana Imani yake kutokana na misingi aliyowekewa, lakini inawezeka katika kuleta maendeleo ya jamii zetu ikiwemo kuelimishana juu ya masuala mbalimbali yanayogusa jamii zetu moja kwa moja.


Ikumbukwe kuwa, zoezi hili linafanyika kwa mara ya pili baada ya lile lililofanyika mwaka jana Jijini Dodoma ikiwa ni maandalizi ya kuelekea kilele cha siku ya Maridhiano Kitaifa itakayofanyika Mkoani Mbeya Machi 6 mwaka huu.






Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa