• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA APEWA TUZO YA UONGOZI ULIOTUKUKA NA WAJUMBE WA ALAT MKOA WA ARUSHA...

Posted on: December 6th, 2023

Na Elinipa Lupembe


Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT), Mkoa wa Arusha, wamemkabidhi Tuzo ya Uongozi Uliotukuka, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John V.K Mongella, mara baada ya kuridhishwa na uongozi wake, unaokwenda sambamba na usimamizi wake thabiti wa utekelezaji wa shughuli za maendeleo mkoani Arusha.


Wajumbe hao, wakiongozwa na Mwenyekiti ALAT Mkoa wa Arusha, na Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha, Mhe. Maximilian Matle Iranghe, wameuelezea uongozi wa Mhe. Mongella, kuwa ni uongozi uliotokuka ndani ya mkoa, uliwaunganisha watu wa Arusha licha ya mgawanyiko wa kisiasa, uliokuwepo kabla ya kupewa dhamana ya kuongoza mkoa huo wa Arusha wenye pilika nyingi za kimaisha.


Mhe. Maximilian, amesema kuwa, wajumbe wa ALAT mkoa,  wameamua kumpa  tuzo hiyo, si kwa ushabiki bali ni kutokana na kuridhishwa na  hali ya utulivu wa wananchi wa Arusha, uliwawezesha kuachana na malumbano ya kisisasa, na kujikita zaidi kwenye shughuli za uzalishaji mali kwa maelendelo ya mtu mmoja mmoja, mkoa na Taifa.


"Arusha ni mkoa wa kimkakati, ukisheheni wakazi wenye heka heka nyingi, uwepo wa uongozi imara wa Mhe. Mongella umeondoa mpasuko uliokiwepo uliotokana na itikadi za kisiasa, na kuthibitisha kuwa Mhe. Mongelle ameweza kuwaunganisha wanaArusha na kuwa kitu kimoja sasa, tunampongeza sana, tunampa maua yake"Amesema


Aidha, amemuelezea Mhe. Mongella ni kiongozi muwazi, asiye na mbili, mara nyingi amekuwa akisema ukweli kwa kupambana, na  kuhakikisha amani na utuivu, huku miradi yote inatekelezwa kwa kuzingatia ubora unaoendana na thamani ya fedha.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Arusha, Mhe. Ojung'u Salekwa, amempongeza, Mhe. Mongella kwa kazi nzuri anayoifanya, na kuhakikisha usalama wa mkoa, unasababisha wananchi wake kujikita kwenye kufanya  shughuli za maendeleo na si malumbano.


Ameweka wazi kuwa, Mhe Mongella amekuwa msimamizi mzuri wa miradi yote ya maendeleo, inayofanyika kwenye halmashauri zake, bila kubagua, akiweka mbele maslahi ya Umma,  ambayo wamekiri na kushuhudia ikitekelezwa na kukamilika kwa wakati, huku ikizingatia viwango vya ubora unaoendana na thamani ya fedha zilizotolewa na serikali.


Hata hivyo Mhe. Mongella amewashukuru Wajumbe hao wa ALAT kwa kuona anastahili kupewa tuzo hiyo, huku akiwataka kuendeleza umoja na mshikamamo miongoni mwao, ili wananchi waige kutoka kwao, kwa kuwa wao ni viongozi wawakilishi wa wananchi.


Amesema kuwa, wananchi wa mkoa wa Arusha, wanatambua na kuthamini umuhimu wa amani na utulivu, ulipo sasa huku wakiejitoa kufanya kazi za kujitafutia kipato jambo ambalo linamuunga mkono kwa vitendo Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, anaye wahimiza waTanzania kufanya kazi, huku ikithibitishwa na agenda yake ya  Kazi Iendee kama kipaumbele chake.


#arushafursalukuki

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa