• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA ASISITIZA  UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, DAWA,  VIFAA NA VIFAA TIBA KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA  AFYA...

Posted on: December 29th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mhe. John V.K Mongella ametembelea na kukagua hali ya utoaji na upatikanaji wa huduma za afya, katika Kituo cha Afya Karatu, na kushuhudia wananchi wakiendelea kupata huduma za afya kama kawaida.

Akiwa kituoni hapo, Mkuu huyo wa mkoa, ameuagiza uongozi wa wilaya ya Karatu, kusimamia hali ya utunzaji na uhifadhi wa dawa, vifaa na vifaa tiba, huku akisistiza dawa ambazo hazijaanza kutumika, kuhamishiwa kwenye famasi kubwa ya hospitali ya Wilaya, hospitali ambayo inalo eneo maalum la kuhifadhia dawa, badala ya kuziacha kituoni hapo ambapo kuna eneo finyu.

Hata hivyo Mhe. Mongella ameendelea kukerwa na hali ya  utunzaji duni wa vifaa na miundombinu na kuwasisitiza watumishi wa Afya, kuwa wazalendo kwa kuthamini na kuvitunza vifaa vyote,  vinavyonunuliwa na Serikali kwa ajili ya kuwahudumia wananchi na sio kuviacha viharibike ovyo.

"Wahudumu wa afya mnalo jukumu la kutunza vifaa na vifaa tiba katika maeneo yenu, ikiwa ni pamoja na kufanya ukarabati mdogo kwa vifaa vinavyohitaji matengenezo madogo madogo badala ya kusubiri viharibike kabisa na kusababisha Serikali kuingia gharama ya kununua upya, jambo ambalo linawezekana kuepukika.

Aidha, amesistiza kuharakisha kutengeneza generata la kituoni ambalo lilipata hitilafu, ili chumba cha kuhifadhia maiti kiendelee kufanya kazi, na kumtaka Mkurugenzi halmashauri ya Karatu kujipanga kukarabati jengo hilo la mochwari.

Hata hivyo, Mganga Mfawidhi Kituo cha Afya Karatu, Dkt. Iman Emmanuel, amesema kuwa,  generata la kituo liliharibika na kupelekwa kwa fundi,  tayari limeshatengenezwa na litarudishwa kituoni hapo kuendelea na kazi, huku akikiri kufanyia kazi maagizo yote yaliyotolewa na Mkuu wa mkoa na kujipanga upya kurekebisha changamoto zilizooneka na kuendelea kutekeleza jukumu lao la kuwahudumia wagonjwa na kufikia malengo ya Serikali

Awali, Mhe. Mongella yupo wilayani Karatu kwa ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa shughuli za  maendeleo kiskta za wilaya hiyo.

#aushafursalukuki

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa