• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA AZUNGUMZA NA WAWEKEZAJI KUTOKA NCHINI VIETNAM

Posted on: December 20th, 2023

Na Elinipa Lupembe.


Wawekezaji wa waTaasisi ya Vietnam Tanzania wakiongozwa na Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Prof. Salmin Ibrahim Salmin, wamefika kwenye ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha na kufanya mazungumzo mafupi na Mkuu wa mkoa huo, Mhe. John V.K.Mongella, leo tarehe 20 Desemba 2023.


Akizungumza kwa niaba ya wawekezaji hao, Prof. Salmin amesema kuwa,  wawekezaji hao wanaojihusisha na miradi ya Kilimo, viwanda vya kusindika  mazao, madini pamoja na kusafirisha bidhaa zitakazozalishwa nje ya nchi, wako mkoani Arusha kwa ajili ya kutafuta eneo la kuwekeza mradi huo.


Amesema kuwa mradi huo, unaotarajiwa kuanza mapema Januari 2024 huku wakia na matarajio ya kushirikiana na wakulima wazawa kwa kuwapa pembejeo za kilimo, mikopo ya vifaa vya kilimo, ujenzi wa nyumba nafuu pamoja na kuwajengea uwezo wa kilimo cha kisasa.


Awali Mhe. Mongella amewakaribisha mkoani humo kwa ajili ya kufanya uwekezaji kama yalivyo malengo yao na kuwaeleza nia thabiti ya Serikali ya awamu ya sita inayongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuweka mazingira ya kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje ya Nchi pamoja na kuwahikikishia mazingira rafiki ya kufanyia shughuli zao.


Amebainisha kuwa, uwekezaji huo ni muhimu kwa mkoa wa Arusha, na zaidi utaleta manufaa kwa taifa kupitia kodi pamoja na kuwanufaisha wananchi kwa kupata ajira na wengine kupata soko la malighafi zao watakazozalisha kutokana na kilimo.


Aidha, amewaahidi ushirikiano mkubwa wawapo Arusha kwa kuhakikisha uwekezaji watakaoufanya, utaleta faida kwa pande zote mbili, kwa nchi na wawekezaji pia.


Hata hivyo, wawekezaji hao, wameishukuru serikali ya Tanzania, mkuu wa mkoa wa Arusha kwa kuwapa fursa ya kuwekeza na kuwakaribisha mkoani Arusha na kuahidi kushirikiana na watanzania kufanya shughuli za uzalishaji kwa manufaa ya wote.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa