• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI YA AWAMU YA SITA IMEWEKA MIKAKATI YA KUHAMASISHA UWEKEZAJI SEKTA YA UTALII NCHINI...

Posted on: April 30th, 2024

Na Elinipa Lupembe

Katika kukuza na kuimarisha Sekta ya Utalii nchini, Serikali ya awamu ya sita imeweka mikakati mbalimbali ili kuhakikisha, wananchi wanafanya uwekezaji mkubwa kwenye sekta hiyo, ikiwa ni pamoja na kutoa msamaha wa ushuru na punguzo la kodi kwa wawekezaji.

Hayo yamewekwa wazi na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini Tanzania, Gilead Terry, alipozungumza na wanahabari, muda mfupi kabla ya kuanza Kongamano la Uwekezaji, linalofanyika kwenye Ukumbi wa mkutano Gran Melia Jijini Arusha, Aprili 30, 2024.

Terry amesema kuwa, kutokana na ongezeko la idadi ya watalii inayotokana na programu ya Tanzania Royal Tour iliyofanywa na Mhe. Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan mwaka 2022, imeandaa Sera inayolinda mtaji wa Mwekezaji kwa kushusha kodi kutoa dola milioni 1 mpaka kufikia laki 5 na dola elfu 50 kwa wazawa huku ikitoa msamaha wa ushuru mpaka pale mtaji utakapoanza kutoa faida.

"Tunataka mtaji wa Mwekezaji utumike kukuza mtaji wake badala ya kulipa mrundikano wa kodi, na kuruhusu kuanza kulipa kodi mara baada ya kutengeneza faida, hali ambayo licha ya kutoa unafuu kwa wawekezaji inasaidia kuvutia wawekezaji wengi zaidi wazawa na wageni kuwekeza kwenye sekta ya Utalii" Amesema Terry

Aidha, ameyataja malengo ya Kongamano hilo ni pamoja na kuwajulisha wadau fursa zinazopatikana kwenye sekta ya utalii na nafuu mbalimbali zilizowekwa na Serikali kupitia sheria ya Uwekezaji ya mwaka 2022 na kusisitiza wawekezaji kuwa huu ni mwaka wa kutengeneza faida kupitia sekta hiyo.

Amefafanua kuwa, Kongamano hilo litatoa fursa ya kuwasilisha fursa, zinazopatikana kwenye sekta ya utalii, mawasilisho yatakayochochea majadiliano kati ya watalamu na wadau waliopo kwenye sekta ya Utalii mkoani Arusha, ili kujua fursa na changamoto zilizopo ili kuongeza kiwango cha uwekezaji kwenye sekta hiyo.

Awali, Kongamano hilo linafanyika kufuatia maagizo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyoyatoa wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali mwanzoni mwa mwezi Aprili, 2024, akimtaka Mkuu wa Mkoa wa Arusha, kushughulikia changamoto ya upatikana wa vyumba vya kulala wageni.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa