• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI YAANZA KUTOA VITAMBULISHO VYA KISASA KWA WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO

Posted on: October 18th, 2024

SERIKALI YAANZA KUTOA VITAMBULISHO VYA KISASA KWA WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO

Uzinduzi Kabambe wafanyika Arusha!

Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imezindua rasmi ugawaji wa vitambulisho vya kidijitali kwa ajili ya wafanyabiashara ndogondogo nchini.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe.Dkt. Dorothy Gwajima akizungumza na wafanyabiashara hao na wananchi wa jijini Arusha wakati akizindua vitambulisho hivyo leo Oktoba 17, 2024, amebainisha kuwa vitambulisho vitakuwa fursa muhimu kwa wafanyabiashara ndogondogo kuwainua kiuchumi.

Amesema Serikali kwa vipindi tofauti imeendelea kushughulikia changamoto za wafanyabiashara ndogondogo na kwa kutambua juhudi hizo, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendeleza juhudi hizo kwa kuzingatia maendeleo ya teknolojia na ukuaji wa uchumi jumuishi.

Waziri Dkt. Gwajima amezitaja baadhi ya juhudi hizo ni pamoja na ujenzi wa ofisi za wafanyabiashara ndogondogo na kuwapanga kwenye maeneo rasmi yaliyotengwa na Serikali ambapo hadi sasa mikoa kumi na mbili (12) imekamilisha ujenzi wa ofisi hizo.

Ametaja pia uboreshaji wa miundombinu unaotekelezwa na Ofisi ya Rais – TAMISEMI, uratibu wa utoaji wa mikopo kwa wafanyabiashara ndogondogo ambapo Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali zimeendelea na jitihada za kuwaendeleza kiuchumi ikiwemo mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri na mikopo kutoka Baraza la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi na Wizara ya Viwanda na Biashara.

"Kwa upande wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imeingia mkataba na Benki ya NMB wenye thamani ya Shillingi Bilioni 18.5 kwa ajili ya kutoa mikopo yenye masharti nafuu kwa wafanyabiashara hao. Vilevile Wizara itaendelea kutumia mfuko wa Maendeleo ya Wanawake (WDF) kuwezesha wanawake wajasiliamali." amesisitiza Waziri Dkt. Gwajima.

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda akizungumza katika tukio hilo, ametoa wito kwa wafanyabiashara ndogondogo kutumia fursa hiyo ya pekee kwao ili kujinufaisha zaidi kiuchumi huku akiwahimiza wananchi wote kushirikiana kutokomeza vitendo vya ukatili kwa  kutoa taarifa za ukatili.



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa