• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI YAFIKISHA UMEME MGODI WA DHAHABU ENDAGEM; WANANCHI WAISHUKURU SERIKALI YA MAMA SAMIA

Posted on: March 9th, 2024


Na Elinipa Lupembe 


Serikali ya awamu ya sita, katika kuhakikisha umeme unafika maeneo yote vijijini kwa lengo la kuchochea kasi ya maendeleo nchini na ukuaji wa wa uchumi, kupitia mradi wa umeme vijijini REA, imefanikiwa kusambaza umeme kwenye  Kijiji cha Endagem kata ya Endabash, wilaya ya Karatu na hatimaye kufikisha kitongoji cha Maurus, eneo la machimbo ya Dhahabu Mgodi wa Endagem.

Wachimba hao wadogo wa madini ya dhahabu, katika mgodi huo, wameishukuru na kuipongeza serikali kwa kusikiliza na kutatua kero za wananchi, kwa kufikisha huduma hiyo kwenye mgodi huo, kero ambayo imedumu kwa miaka 12, kero ambayo waliiwasilisha kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.John V.K Mongella Oktoba, 2023 na muda mfupi tayari umeme umefika eneo hilo.


Akizungumza kwa niaba ya wachimbaji hao, Mwenyekiti wa wachimbaji Madini ya dhahabu Mgodi wa Endagen, Abdul Amir Mwangu, amekiri uwepo wa rasilimali ya umeme eneo hilo, utaongeza kasi ya uchimbaji utakaokuza biashara na pato la mtu mmoja mmoja kwa wachimbaji hao, kwa kuwa sasa watachimba madini kwa kutumia mashine zenye teknolojia ya kisasa zinazotumia umeme, tofauti na hapo awali walichimba kwa mashine duni zilizotumia mafuta ya dizel ambazo zinatumia gharama kubwa za uendeshaji.


"Tunaishukuru Serikari ya Mama Samia, ametimiza haja na matamamio yetu ya miaka mingi, tulitoa kero yetu mwezi Oktoba, 2023 kwa mkuu wa Mkoa, muda mfupi tumepata umeme na transfoma mbili kubwa zimesimikwa eneo hili, tumeshuhudia Serikali ya awamu ya sita kuwa ni sikivu, tunaamini tunakwenda kuongeza kasi ya uzalishaji kwa kutumia mashine za kisasa,  tumekuwa tukichimba kwa teknolojia dhaifu iliyozorotesha uzalishaji kwa sasa biashara zetu zinakwenda kukua". Amesema Menyekiti Mwangu.


Hata hivyo wananchi hao, licha ya kuishukuru Serikali,  wameiomba kujengewa shule ya msingi na zahanati kwa kuwa eneo hilo halina huduma hizo, jambo ambalo linawatesha wanawake wajawazito na watoto wadogo wasio na uwezo wa kutembea umbali mrefu kufuata shule kijiji cha Laja.


Akiwasilisha taarifa ya Mradi huo, Meneja wa TANESCO Karatu,Mhandisi Henry Chahe, amesema kuwa, mradi huo unaotekelezwa kwa gharama ya shilingi milioni 545.3, umetekelezwa na kampuni ya ETDCO kampuni tanzu ya TANESCO na umefikia asilimia 80, 


Kiasi hicho cha fedha, kimehusisha ujenzi wa laini kubwa ya umeme wenye urefu wa Km 10, ujenzi wa laini ndogo za Km 5 na kuzunguka eneo lote katika mashimo ya migodi pamoja na kufunga Mashine umba 2 za ukubwa wa KVA 200 33/0.4KV (transfomer 2).


#arushafursalukuki 




                        
                       
                        </div>
                        <!-- /.right-sidebar-content -->
                        <!--/END RIGHT SIDEBAR CONTENTE SECTION-->
                    </div>



<div class=

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa