• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI YAJA NA MFUMO WA KUSAJILI VITAMBULISHO VYA MACHINGA KIDIGITALI.

Posted on: February 19th, 2024


Kufuatia mkakati wa Serikali wa Kuwasajili Wajasiriamali maarufu kama machinga Kidigitali, imeanza kutoa mafunzo kwa Maafisa TEHAMA, Maendeleo ya Jamii na Biashara kutoka halmashauri za Mkoa wa Arusha, ili waanze kuwasajilijili wafanyabiashara hao wadogo.


Mfumo huo utakaowezesha wajasiriamali wote, kutambuliwa, kusajiliwa na kupata Vitambulisho vya Kidijitali vitakavyowawezesha kutambulika rasmi na kunufaika na fursa za kibiashara zilizopo.


Akifungua Mafunzo hayo kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Missaile Albano Musa, Katibu Tawala Msaidizi, Mipango na Uratibu, Apolinary Seiya, amewataka Maafisa hao kufuatilia kikamilifu mafunzo hayo ili kupata ujuzi na maarifa yatakayowawezesha kufanya zoezi hilo la kitaifa kwa weledi mkubwa na kufikia malengo ya Serikali ya kuwatambua wajasiriamali rasmi kwenye mfumo wa kidijitali iliyoainishwa.


Amesema kuwa, mafunzo hayo ni utekelezaji wa adhima ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwawezesha wajasiriamali kutambulika rasmi ili waweze kunufaika na fursa rasmi zinazotolewa na Serikali kupitia taasisi za kifedha kama vile mikopo yenye riba nafuu.


"Mfumo wa Utambuzi na usajili wa kutoa vitambulisho kwa wafanyabiashara ndogondogo umekamilika baada ya kufanyiwa maboresho makubwa ili uweze kupata vitambulisho vya kidigitali, niwatake sasa mkafanye zoezi hili kwa weledi mkubwa katika maeneo yenu bila kutoa upendeleo kwa mfanyabiashara yeyote." Amesema Seiya


Mfumo wa utambuzi, Usajili na utaoji wa vitambulisho utawezesha kuwatambua, kuwasajili na kuwapa vitambulisho vilivyounganishwa na mfumo wa NIDA, vitambulisho ambavyo vitawapa fursa ya wajasiriamali ya kupata mikopo yenye masharti nafuu kutoka taasisi za fedha.


Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Juliana Mtolela amesema kuwa, vitambulisho hivyo vitakuwa tofauti na vile vya zamani kwani vitakuwa vya kidigitali na vitakuwa na taarifa zote za muhimu za mfanyabiashara zikiwa zimeunganishwa na taarifa za vitambulisho vya NIDA na kumfanya kutambulika rasmi na Serikali pamoja na Taasisi zingine za kifedha.


Hata hivyo, washiriki wa mafunzo hayo wamethibisha kuwa mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka yanayokwenda kuwezesha kutambua mahitaji ya wajasiriamali  na kutafuta namna bora ya kuwahudumia.


"Tunashukuru sana Serikali kuwezesha mafunzo haya kufanyika, yatatusaidia kupata takwimu sahihi ya wajasiriamali na wamachinga kwaajili ya kuwa na njia sahihi ya kutatua changamoto zinazowakabili sambamba na wao kunufaika na fursa mbalimbali za mikopo kutoak taasisi za fedh." Amesema Afisa Bishara Wilaya ya Monduli, Edna Fransis.


Ikumbukwe kuwa, mafunzo hayo ya mfumo huo ni ahadi ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa 25 Januari, 2022 ya kuunda mfumo rasmi wa  kuwatambua wajasiriamali  wadogo Kidigitali ili watambulike katika mfumo rasmi.


#arushafursalukuki



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa