• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI YAPATA MWAROBAINI WA KUONDOA  MAJUNGU NA UONEVU KWA WATUMISHI...

Posted on: December 17th, 2023

Na Daniel Gitaro


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora , Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema matumizi ya mfumo wa PIPMS, PEPMIS na HR Assessment katika Utumishi wa Umma nchini unaenda kuondoa tabia ya majungu na uonevu katika  Utumishi wa Umma huku akiwataka watumishi wa umma nchini kuupokea kwa mikono miwili mfumo huo.


Mhe. Kikwete ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Meru Mkoani Arusha,  ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kikazi ya kukagua mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa Kupima Utendaji Kazi wa Watumishi wa Umma na Taasisi (PEPMIS na PIPMIS) na Mfumo Maalum wa Tathmini ya hali ya Rasilimali watu Serikalini (HR Assessment) yanayoendelea kufanyika mkoani humo.


Amesema mfumo wa OPRAS uligubikwa na udanganyifu, uonevu na upendeleo miongoni mwa watumishi, hivyo Serikali imekuja na mfumo wa kielektoniki ili kupunguza malalamiko ya watumishi wa Umma.


Kufuatia hatua hiyo, Mhe. Kikwete amewataka Watumishi wa Umma nchini, kufurahia ujio wa mifumo hiyo mipya  kwani itatoa haki kwa wote na kuwafanya viongozi na watumishi wa Umma kwa ujumla kutekeleza majukumu yao kiuhalisia, tofauti na ilivyokuwa kwenye mfumo wa OPRAS.


Amefafanua kuwa  mfumo wa PEPMIS na PIPMIS ni mwarobaini wa masuala yote yaliyokuwa yakilalamikiwa na itasaidia kwa watumishi kupandishwa vyeo  kwa wakati.


Amesema kuna baadhi ya watumishi kazi yao kubwa wakifika maofisini, ni kuangalia nani kafika saa ngapi pamoja na kuchukua maneno huku na kupelekwa kwa wakuu wao ili mradi tu wapendwe.


Katika hatua nyingine, Mhe. Kikwete amesema mifumo hiyo mipya inakwenda kumlazimisha Mtumishi kutekeleza majukumu yake kwa fani aliyosomea na sio vinginevyo la sivyo mfumo huo utashindwa kumtambua.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru, Mwl. Zainab Makwinya amesema mifumo hiyo imekuja wakati muafaka kwani itatoa nafasi kwa watumishi kwenda kuwahudumia wananchi na sio kukaa maofisini.


Ameongeza kuwa  mfumo huo  utabaini watumishi wanaokwenda maofisini kusaini tu ili waonekane wapo na wale wanaokwenda ofisini kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.


#ArushaFursaLukuki

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa