• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TAASISI ZA FEDHA ZATAKIWA KUIMARISHA MIFUMO YA KUWALINDA WATUMIAJI...

Posted on: November 22nd, 2023


Na Prisca Libaga


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Fedha iimarishe mifumo ya kuwalinda watumiaji wa huduma za fedha ili baadhi ya watoa huduma wasio waadilifu wasitumie changamoto ya uelewa mdogo wa masuala ya fedha kwa baadhi ya wananchi na kuwadhulumu.


Pia, Mheshimiwa Majaliwa amesema Wizara ya Fedha iendelee kushirikiana na na watoa huduma za fedha kutoa elimu kwa wananchi katika maeneo muhimu yakiwemo ya usimamizi wa fedha binafsi, kuweka akiba, mikopo, uwekezaji kupitia hatifungani na hisa, bima, mpango wa kujiandaa na maisha ya uzeeni pamoja na kodi.


“Wizara ya Fedha iandae mpango maalumu wa kutoa hamasa kwa Watanzania ili wajenge utamaduni wa kutumia huduma rasmi za kifedha, pia elimu iendelee kutolewa kuhusu wajibu wa kila mmoja kudai na kutoa risiti kwa malipo yanayofanyika. “


Ametoa maagizo hayo leo Novemba 22, 2023 alipofungua Wiki ya Huduma ya Fedha Kitaifa, jijini Arusha, ambapo ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa watoa huduma za kifedha wapunguze gharama za upatikanaji wa huduma za fedha zikiwemo riba na ada ili wananchi wengi watumie huduma za fedha zilizo rasmi.


Pia, Mheshimiwa Majaliwa ameisisitiza Wizara ya Fedha iendelee kusimamia na kuratibu utekelezaji wa Programu ya kutoa elimu ya fedha kwa umma na kuhakikisha kuwa elimu hiyo inawafikia wananchi wengi zaidi mijini na vijijini.


Waziri Mkuu amesema Wizara ya Fedha inatakiwa iandae mpango maalumu wa kutoa hamasa kwa Watanzania ili wajenge utamaduni wa kutumia huduma rasmi za kifedha pamoja na kuratibu gharama za huduma za fedha. “Pia, elimu iendelee kutolewa kuhusu wajibu wa kila mmoja kudai na kutoa risiti kwa malipo yanayofanyika.“


Waziri Mkuu amesema watoa huduma za kifedha hawana budi kujenga uelewa wa kutosha kwa wananchi kabla ya kufunga nao mikataba, pamoja na kuwafafanulia taratibu na masharti yao kabla hawajatoa kwao huduma hizo za fedha. Pia amewataka watoa huduma hao waweke mkakati mahususi wa kuongeza matumizi huduma kwa njia ya kidijitali pamoja na kuzisogeza hadi maeneo ya pembezoni na vijijini ili wananchi walio wengi wanufaike.


“Watoa huduma za fedha ongezeni ubunifu katika utoaji wa huduma. Toeni huduma zinazoendana na wakati, mahitaji ya soko na kuzingatia uhitaji wa makundi mbalimbali katika jamii. Suala hili liende sambamba na kuwaunganisha wajasiriamali na fursa mbalimbali zinazotolewa na sekta ya fedha katika kukuza na kuimarisha biashara zao. “


Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amewataka wasimamizi wa Sekta ya Fedha na wadau wengine wazingatien sheria na kanuni za kuwalinda watumiaji wa huduma za fedha ikiwemo kutatua malalamiko na migogoro na kulipa fidia na mafao kwa wakati.


Amesema lengo la maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa na Maonesho ya Huduma za Fedha yamejikita katika kujenga uelewa kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi ya huduma za fedha zinazotolewa, kusimamia vizuri rasilimali fedha ikiwa ni pamoja na kuimarisha utamaduni wa kujiwekea akiba, kukopa kutoka vyanzo salama na njia sahihi za kulipa madeni ili kujenga uchumi na kuondoa umaskini.


Naye, Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inaendelea kukuza uelewa kwa Watanzania kuhusu masuala ya kifedha huku akitoa wito kwa Watanzania kuweka utaratibu wa kusoma vigezo na masharti ya huduma za kifedha wanazopata kutoka katika taasisi mbalimbali za kifedha ili kuepuka changamoto zinazoweza kujitokeza baadae.


"Ni vyema tukaweka utaratibu wa kusoma na kuelewa vigezo na masharti tunapokuwa tunapatiwa huduma za kifedha hasa mikopo ili tujiepushe kuingia kwenye mikopo yenye masharti magumu ambayo wakati mwingine tunaweza kushindwa kuyatekeleza."


Kwa Upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Bi. Natu El-maamry amesema maadhimisho hayo ya tatu ni muendelezo wa jitihada za Serikali katika kuongeza uelewa wa masuala fedha kwa Watanzania ili waweze kuwa na uelewa kuhusu matumizi sahihi ya huduma za kifedha.


Amesema taasisi mbalimbali za kifedha na wadau wa kisekta wanatumia kipindi hiki kutoa elimu na huduma kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa