• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TANAPA WAHAKIKISHIWA KUPEWA VIFAA VYA KISASA KWA AJILI YA ULINZI WA MALIASILI

Posted on: October 30th, 2023

Na Prisca Libaga


Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angellah Kairuki amesema kuwa Serikali itaendelea kuwaunga mkono TANAPA kuhakikisha wanapata vifaa vingi vya kisasa kwa ajili ya ulinzi wa maliasili ili kukuza utalii katika Hifadhi za Taifa.


Kikao cha Waziri Kairuki pamoja na maafisa na askari hao kimefanyika leo tarehe 28.10.2023 katika Makao Makuu ya Shirika hilo yaliyopo mtaa wa Majengo jijini Arusha.


Mhe. Kairuki alisema, “Serikali itawaunga mkono TANAPA kuhakikisha mnapata vifaa vya kisasa kwa ajili ya kuimarisha doria ili uhifadhi uwe endelevu kwa manufaa ya sasa na baadae”.


“TANAPA mmepewa asilimia 10.2 ya ardhi yote ya Tanzania kuilinda na kuiendeleza. Katika eneo hilo tuhakikishe hakuna uvamizi wa makazi wala mifugo”, aliongeza Mhe. Kairuki.


Waziri Kairuki pia, amelitaka Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kuendelea kuimarisha ujirani mwema kwa vijiji vinavyozunguka hifadhi ili kuwa na uhifadhi wa pamoja na kupunguza migogoro baina ya wananchi na hifadhi.


Aidha, Mhe. Kairuki ametoa wito kwa Watanzania na wasio watanzania kujitokeza kushiriki katika tukio la kupanda Mlima Kilimanjaro ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 62 ya Uhuru wa Taifa la Tanzania.


Waziri huyo alisema, “ninawaomba watanzania kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kupanda Mlima Kilimanjaro, zoezi hilo huwa linaongozwa na JWTZ na wenzetu wa TANAPA. Najua mwaka jana kulikuwa na wapandaji zaidi ya 200, mwaka huu tutavunja rekodi kutokana na kampuni zilizopewa dhamana ya kupandisha watu mlimani kuwa 3 tofauti na mwaka jana ilikuwa ni kampuni 1 tu”.


Kaimu Kamishna wa Uhifadhi TANAPA -Juma Kuji alisema kuwa ziara ya Waziri wa Maliasili na Utalii imekuwa na tija kwa kuendelea kutusisitiza tufanye kazi kwa bidii na kwa kufuata sheria na taratibu.


Kamishna Juma alisema, “kwa niaba ya maafisa na askari wa TANAPA tunakupongeza kwa kuteuliwa kwako na Mhe. Rais na tunakuahidi kuwa maelekezo yako tutayatekeleza ili kuendeleza uhifadhi na kukuza utalii nchini”.


Katika ziara hiyo Waziri Kairuki ameweka wazi nia na mpango wake wa kutembelea Hifadhi zote za Taifa ili kujionea vivutio vya utalii na kuzungumza na watumishi.


Mwisho.



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa