• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TATHIMINI YA USIMAMIZI WA HUDUMA ZA AFYA MSINGI KUFANYIKA KILA BAADA YA WIKI MBILI - Dkt. Magembe

Posted on: November 11th, 2024


Na. James Mwanamyoto Ofisi ya Rais - Tamisemi 


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-TAMISEMI (Afya) Dkt. Grace Magembe amewaelekeza watumishi wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI kuhakikisha wanafanya vikao kazi kila baada ya wiki mbili ili kuboresha usimamizi wa utoaji wa huduma ya afya msingi nchini.



Dkt. Magembe ametoa maelekezo hayo leo wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI kilicholenga kuhimiza uwajibikaji katika eneo la usimamizi wa utolewaji wa huduma za afya msingi nchini.



“Ili kutekeleza kikamilifu majukumu ya idara ya afya, naelekeza kukutana kila baada ya wiki mbili kwa ajili ya kujadili changamoto zinazotukabili, kuanisha shughuli tulizozitekeleza vizuri na kufanya tathmini ya utendaji kazi wetu ili kuwa na ufanisi endelevu wa utekelezaji wa majukumu ya idara yetu,” Dkt. Magembe amesisitiza.



Dkt. Magembe amesema, wananchi wanaotibiwa katika ngazi ya afya ya msingi ni kati ya asilimia 77 hadi 80 hivyo jukumu la Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI ni kubwa kwasababu inawahudumia wananchi wengi walio katika mamlaka ya Serikali za Mitaa.



“Tunawafikia wananchi wengi na si tu kwenye eneo la tiba bali ni pamoja utoaji wa huduma za chanjo, uzazi wa mpango, lishe na ustawi wa jamii, hivyo huduma nyingi wananchi wanazipata kupitia ngazi ya afya ya msingi na hii ni kwasababu zahanati, vituo vya afya na hospitali za wilaya ndio zipo karibu na wananchi,” Dkt. Magembe amefafanua.



Dkt. Magembe ameongeza kuwa, kwa kuwa sehemu kubwa ya wananchi wanategemea huduma katika ngazi ya afya ya msingi hivyo ni muhimu kwa watumishi wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kuhakikisha huduma zinazotolewa zinakuwa na ubora unaotakiwa, zinakidhi matarajio ya wananchi na zinapatikana muda wote. 



“Ninyi na mimi ndio tumepewa jukumu la kuhakikisha tunasimamia na kuratibu utekelezaji wa afua zote za sekta ya afya, kutekeleza maagizo na maelekezo ya viongozi, kuwasimamia vema watumishi wa sekta ya afya walio katika ngazi ya afya ya msingi ili watoe huduma bora, ikiwa ni pamoja pamoja na kupokea maoni na kero wananchi dhidi ya huduma zinazotolewa,”  Dkt. Magembe amehimiza.



Sanjari na hilo, Dkt. Magembe amewataka watumishi wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kuwa na mawasiliano ya kila siku na watumishi wa sekta ya afya walio katika ngazi ya msingi ili kutatua changamoto wanazoweza kukabilisana nazo wakati wa kuwahudumia wananchi.



Dkt. Magembe amefanya kikao kazi na watumishi wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji ikiwa ni pamoja na kufanya tathmini ya utekelezaji wa maazimio ya kikao kazi cha Septemba 17, 2024 kilicholenga kuimarisha usimamizi wa huduma za afya msingi nchini.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa