• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TENDENI HAKI KWA WASAFIRISHAJI_ PROF MBARAWA

Posted on: June 6th, 2022

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa, amewataka wasimamizi wa mizani inayosomamiwa na Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), kutenda haki kwa wasafirishaji hasa wanapokutwa na makosa ya kuzidisha uzito.

Waziri Prof. Mbarawa amesema hayo mkoani Arusha wakati wa sherehe ya ufunguzi wa mizani ya kisasa ya Kimokouwa uliopo wilayani Longido ambayo itatumika kwa ajili ya kupima uzito wa magari yanayofanya safari zake kati ya Tanzania na nchi jirani ya Kenya.

“Sheria inayosimamia mizani ya Afrika Mashariki ni kali sana na ina tozo kubwa hivyo hakikisheni mizani zinakuwa katika vipimo sahihi ili kuondoa mkanganyiko wa uwiano za mizani unaojitokeza mara kwa mara”, amesema Prof. Mbarawa.

Aidha, Prof. Mbarawa amekema vitendo vya rushwa vinavyofanywa na baadhi ya wasimamizi wa mizani kwani athari ya kumuandikia msafirishaji tozo ni kubwa na nyingine zinagharimu zaidi ya gharama ya gari husika.

“Angalieni namna bora ya kuelemisha kwani unakuta gharama ya tozo ni kubwa kuliko hata thamani ya gari husika na kwa mujibu wa sheria lazima itozwe tozo” amefafanua Prof. Mbarawa.

Waziri Mbarawa ametoa agizo kwa TANROADS kuhakikisha wanaendelea kutoa elimu za mara kwa mara kwa watumishi wa mizani, wasafirishaji na madereva kuhusu sheria ya mizani na pamoja na kufanya tafiti kujua tatizo la kutokuwa na uwiano sawa wa uzito wa gari kutoka mizani moja hadi nyingine.

Awali akitoa taarifa ya mradi huo, Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Eng. Rogatus Mativila, amesema kuwa mizani hiyo inayopima magari pande zote mbili za barabara umegharimiwa na Serikali kwa gharama ya shilingi Bilioni 14.7.

Ameeleza kuwa mradi huo upo katika barabara kuu ya Arusha – Namanga ambayo ni sehemu ya barabara kuu ya kimataifa inayojulikana kwa jina la The Great North Corridor  ambapo mtu anaweza kusafiri kutoka Cairo, Misri kupitia Nairobi – Arusha –  Babati – Dodoma – Iringa – Tunduma hadi Cape town, Afrika ya Kusini.

Ameongeza kuwa kukamilika kwa mizani huo kutaondoa ucheleweshaji wa magari wakati wa upimaji uzito pamoja na kupunguza muda wa kusafiri hasa kwa magari ya mizigo yanayokwenda au kutoka nje ya nchi na kuongeza uwazi katika utendaji kazi na hivyo kupunguza malalamiko kutoka kwa wadau wa usafirishaji.

Eng. Mativila ameeleza kuwa mradi huo umejengwa na kampuni ya CRJE (East Africa) na kusimamiwa na Ambicon ya Dar es Salaam.

Mizani ya Kimokouwa ilianza kujengwa mnamo tarehe 11 Mei 2020 kwa lengo la kudhibiti uzidishaji uzito wa magari yanayotumia barabara Kuu ya Arusha-Namanga ili kuwezesha miundombinu ya barabara kudumu kwa muda uliokusudiwa wakati wa usanifu wake.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa