• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TUFANYE KAZI KWA UMOJA

Posted on: July 5th, 2020

Viongozi wa Taasis za Serikali Mkoani Arusha, wametakiwa kufanya kazi kwa umoja na mshikamano, katika kuhakikisha wanatoa huduma shahiki kwa wananchi.

Maelekezo hayo yametolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mheshimiwa Idd Kimanta alipokutana na viongozi hao na kujitambulisha kwao kama kiongozi wao mpya, jijini Arusha.

“Siri kubwa ya mafanikio ni kufanya kazi kwa umoja na kujenga hali shirikishi katika taasis zenu ndipo mtakapoweza kufikia malengo mliojipangia”.

                                                                          Baadhi ya viongozi kutoka taasis mbalimbali za serikali mkoani Arusha, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Arusha (Hayupo pichani) katika

                                                                                kikao kazi kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha.


Mheshimiwa Kimanta amewashauri kutopenda kutumia lugha za umri sana kwa wasaidizi wao, bali watumie mbinu ya kujenga mahusiano mazuri ya kazi kwani hata wao wanajitambua na wanaelewa wajibu wao katika kutekeleza majukumu yao.

Amewataka viongozi hao wakafanye kazi kwa utulivu, na ili waweze kufanikisha hilo wajitaidi kupata taarifa nyingi zinazohusu taasis zao na wasaidizi wao ambazo zitawasaidia kujenga zaidi nguvu na mshikamano.

Pia, amewashauri kwenda kusimamia misingi na taratibu za uongozi wa taasis zao bila kuogopa changamoto zozote zitakazoibuka na wakishindwa basi wasisite kumshirikisha yeye kwa msaada zaidi.

Amesisitiza zaidi kuwa kila kiongozi wa taasis ya serikali ni mteule wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo hawana budi kuhakikisha wanatekeleza yale yote ambayo Rais anayataka katika kuleta maendeleo ya nchi.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Arusha mheshimiwa Kenan Kihongosi, amesema yote yaliyozungumzwa na Mkuu wa Mkoa ni maelekezo kwa viongozi wote wa serikali hivyo wanatakiwa kuyafanyia kazi.

Aidha, amewataka viongozi hao wa taasis za serikali kuchukua hayo maelekezo na kuyafikisha kwa wasaidizi wao wa ngazi za chini hii itasaidia kuongeza ufanisi zaidi mahala pao pa kazi.

Mkurugenzi wa huduma za ufundi kutoka taasis ya utafiti wa viwatilifu katika ukanda wa Kitropiki (TPRI) daktari Efrem Njau, amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuwapa muongozi mzuri wa namna ya kufanya kazi kwa umoja katika mkoa wa Arusha.

Daktari Njau amesema, watawashirikisha wanao waongoza yale yote walioelekezwa na Mkuu wa Mkoa kwa kuongeza ufanisi zaidi katika taasis zao.

                                                                   Mkurugenzi  wa Huduma za Ufundi kutoka Taasis ya Utafiti wa Viwatilifu katika Ukanda wa Kitropiki, Daktari

                                                                              Efrem Njau, akizungumza katika kikao kazi cha wakuu wa Taasis za serikali za Mkoa wa Arusha,jijini Arusha.

Mkurugenzi kutoka walaka wa barabara(TANROAD) Arusha, Inginia Johnny Kalupale amesema, wao kama viongozi wa taasis za serikali wapo tayari kutoa ushirikiano kwa Mkuu wa Mkoa ili kuhakikisha Mkoa unatekeleza yale yote ambayo Mheshimiwa Rais anayataka.

Mheshimiwa Kimanta amekutana na viongozi hao wa taasis za serikali kwa lengo kubwa la kujitambulisha kwao na kuwapa muongozo wa namna ya kutekeleza majukumu yao ndani ya Mkoa wa Arusha.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa