• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TUNZENI VYANZO VYA MAJI

Posted on: November 23rd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, imeiagiza bodi ya Mamlaka ya maji safi na Usafishaji Mazingira ya jiji la Arusha AUWSA kuweka kipaombele katika utunzaji wa vyanzo vya maji viliyopo katika mlima Meru.

Ameyasema hayo alipokuwa  katika ziara yake ya ukaguzi wa miradi ya maji katika jiji la Arusha.

“Nimewahi kusikia wataalam wa maji wakisema Vita ya Tatu ya dunia itahusisha kugombea maji,ninaomba sisi tuanze kujihami kwa kutunza vyanzo vyetu vya maji.Niitake bodi ya AUWSA kuandika andiko la mradi ambalo tutalipigia debe katika ofisi ya Makamu wa Rais inayoshughulikia Mazingira ili kuweza kupata ufadhili wa kampeni yetu hii ya utunzaji wa vyanzo vya maji”.

Gambo alisema,itakuwa haina maana kutumia kiasi kikubwa cha fedha za serikali katika uboreshaji wa huduma za maji na baada ya miaka michache ijayo vyanzo vyote vikauke.

Nae Mkurugenzi wa Mmlaka ya Maji safi na usafirishaji (AUWSA) Mhandisi Ruth Koya amesema, mradi huo utakamilika June 2020 na Arusha itanufaika sana na mradi huo kwakuwa  ukosefu wa maji utakuwa historia.

Amesema tayari wakandarasi wameshaanza kusambaza mtandao wa maji safi na taka kwa kuweka mabomba ya kisasa yanayoendana na mahitaji ya sasa.

Aidha, amesema mpaka mradi huu ukamilike upatikanaji wa maji katika jiji la Arusha utafikia asilimia 100 tofauti na hali ya sasa ambapo ni asilimia 44 tu ya wananchi ndio wanapata maji safi.

Ruth alisema, uzalishaji wa maji utaongezeka kutoka wastani wa lita milioni 40 hadi lita milioni 200 kwa siku na upotevu wa maji utashuka toka asilimia 40 za sasa hadi wastani wa asilimia  25.

Mwenyekiti wa bodi ya AUWSA, Dk. Richard Masika ameipongeza serikali ya awamu ya tano kwa kuweza kutoa fedha kiasi cha shilingi bilioni 520 kupitia mkopo wa riba nafuu kutoka benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika kufanikisha mradi huu mkubwa na ametoa rai kwa wananchi wa Arusha kuitunza muindombinu iliyopita katika maeneo yao kwa ajili ya manufaa ya leo na baadae.

Gambo yupo katika ziara ya siku 3 katika wilaya ya Arusha, Arumeru na Longido akikagua miradi ya maji inayoendeleo katika maeneo hayo.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa