• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TUTAWACHUKULIA HATUA WATUMISHI WANAOKIUKA SHERIA UKUSANYAJI MAPATO’ MCHENGERWA...

Posted on: May 14th, 2024

OR-TAMISEMI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema serikali haitavumilia ukiukwaji sheria na hatua kali zitachukuliwa kwa watumishi watakaobainika kukiuka sheria kwenye ukusanyaji mapato ya serikali.


Mhe.Mchengerwa ameyasema hayo bungeni leo alipokuwa akitoa ufafanuzi wa malalamiko yaliyotolewa bungeni wiki iliyopita na Mbunge wa Msalala (CCM), Idd Kassim kuwa Mamlaka za Seikali za Mitaa zinatoza ushuru mashambani na wafanyabishara wasiolipa wanapewa adhabu kali na kupigwa.


Akitoa ufafanuzi, Waziri Mchengerwa ameliambia bunge kuwa ushuru wa mazao hutozwa kwa Mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura ya 290 na vifungu vya 6,7,8 na 9 vya sheria hiyo ushuru wa mazao ni moja ya vyanzo vya mapato kwa mamlaka za miji, halmashauri za wilaya, mamlaka za miji midogo na halmashauri za vijiji.


Aidha, amesema kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa,Sura ya 290 ushuru huo unatozwa kwa asilimia tatu ya bei ya kununulia shambani kwa mazao ya chakula na biashara.


“Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura ya 290, inatamka kuwa ushuru huu unalipwa na mnunuzi wa zao alilonunua kutoka kwa mkulima kwa kiwango cha asilimia tatu ya bei ya kununulia shambani, endapo mfanyabiashara atanunua mazao hayo kutoka shambani kwa mkulima, atapaswa kulipa ushuru huo katika eneo hilo ambalo ununuzi umefanyika,”amesema.


 Kadhalika, amesema ununuzi ukifanyika sokoni ushuru utatozwa katika soko hilo. Aidha, mazao yanapotoka nje ya Halmashauri yanapaswa kuwa yamelipiwa ushuru na endapo itabainika mfanyabiashara anayetoa mazao nje ya Halmashauri pasipo kuwa na risti halali ya malipo ya ushuru, atapaswa kulipa ushuru wa mazao husika na faini.


“Aidha Mkulima anayesafirisha mazao chini ya tani moja amesamehewa kulipa ushuru huo. Ninaomba kutoa rai kwa Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kusimamia sheria hiyo kwa kuzingatia maslahi mapana ya pande zote mbili, yaani upande wa mnunuzi na upande wa mnunuzi na upande wa Halmashauri’ amesema

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa