• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WAAJIRI WAPENI KAZI MAAFISA UNUNUZI NA UGAVI WALIOSAJILIWA NA BODI YA PSPTB KAMA SHERIA ZINAVYOELEKEZA...

Posted on: December 12th, 2023

Na Mwandishi wetu



Serikali imewaagiza waajiri wa Sekta zote nchini, kuhakikisha wataalam wanaofanya kazi za Ununuzi na Ugavi wanakuwa na sifa sitahiki, kama ilivyoainishwa kwenye Sheria Na. 23 ya mwaka 2007 iliyoanzisha Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), pamoja na miongozo inayotolewa.

Maagizo hayo yametolewa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), wakati akifungua Kongamano la 14 la Wataalam wa Ununuzi na Ugavi linalofanyika kwenye Kituo cha Mikutano ya Kimataifa Arusha (AICC) mkoani Arusha na kusisitiza watalaam wa Ununuzi na Ugavi kuhakikisha wanasajiliwa na Bodi ya (PSPTB), kama inavyoelekezwa.

Dkt. Nchemba ameweka wazi  kuwa, wapo watalam wa fani hiyo, wanaofanya kazi kwenye taasisi za serikali bila kusajiliwa na Bodi ya (PSPTB), jambo ambalo linasikitisha kwa kuwa tayari lipo takwa la kisheria katika kifungu cha 11 cha Sheria ya PSPTB, linaloanisha sifa stahiki za Afisa Ununuzi na Ugavi.

“Changamoto ya kuwapo kwa wataalam ambao wanafanyakazi pasipo sifa stahiki kwa sehemu kubwa inachangiwa na waajiri kuruhusu kazi za ununuzi kufanywa na waajiriwa nje ya taaluma ya ununuzi na ugavi ambayo kwa ukubwa wake inazigusa Ofisi ya Rais TAMISEMI yenye watumishi wengi zaidi wa kada hii, Ofisi ya Rais Utumishi ambao wanasimamia masuala ya ajira pamoja na Wizara Fedha kama mlezi wa kada ya ununuzi na ugavi”, alieleza Dkt. Nchemba.

Dkt. Nchemba alimwelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Fedha kushirikiana na Bodi ya PSPTB, kukutana na Katibu Mkuu TAMISEMI, Katibu Mkuu Utumishi kwa utatuzi wa changamoto hiyo ili kuhakikisha kazi za ununuzi na ugavi zinafanywa na wataalamu wenye sifa na waliosajiliwa na Bodi kwa mujibu wa Sheria ya PSPTB. na sio vinginevyo.

Aidha, Dkt. Nchemba alimwelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Fedha kuangalia uwezekano wa kuisaidia PSPTB kupata fedha ili iweze kufanikisha majukumu ya utekelezaji wa baadhi ya majukumu yake kisheria ikiwa pamoja na kufanya ukaguzi wa wataalam wake nchi nzima katika sekta ya umma na sekta binafsi.

Vile vile Bodi hiyo iweze kuwajengea uwezo wataalam na wadau kwenye mnyororo wa ununuzi na ugavi na kufanya utafiti wa kitaaluma unawoweza kuleta ufumbuzi wa usimamizi bora wa mnyororo wa ununuzi na ugavi mambo ambayo hayafanyiki ipasavyo kwa sababu ya ufinyu wa bajeti.

Kongamano hilo la 14 litafanyika kwa siku tatu likiwa na Kauli mbiu ya "Mabadiliko ya kidigitali  katika kuboresha usimamizi  wa mnyororo wa manunuzi na ugavi kwa maendeleo Endelevu"

#arushafursalukuki

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa