• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WAATHIRIKA WA MAPOROMOKO YA TOPE HANAN'G WAKABIDHIWA NYUMBA ZA KUISHI

Posted on: December 20th, 2024

Na Elinipa Lupembe 



Familia zilizoathirika kufuatia maporomoko ya matope yaliyotokea wilaya ya Hanan'g eneo la Kateshi mkoani Manyara, maafa yaliyotokea Desemba, 2023, na kusababisha baadhi ya watu 700 kukosa makazi, wamekabidhiwa nyumba za kuishi na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa leo, Desemba 20, 2024 kwenye kitongoji cha Waret.



Mhe.Majaliwa amekabidhi nyumba 109 kwa waathirika wa maafa hayo na akisisitiza kuwa hiyo ni ishara ya upendo na kujali kwa Mhe.  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.



Akizungumza mara baada ya kukabidhi na kuzindua nyumba hizo, Waziri Mkuu amesema kuwa Mhe. Rais ametoa pole kwa waathirika wote na amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwaunga mkono ili waweze kurejesha mfumo wa maisha yao kama ilivyokuwa awali.



"Ujenzi wa nyumba 73 kati ya 109 umegharamiwa na Serikali Kuu na kujengwa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA-JKT), nyumba nyingine 35 zimejengwa na Shirika la Msalaba Mwekundu Tanzania huku nyumba moja ikijengwa na Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Taifa (UWT)" amebainisha.



Ameongeza kuwa, kufuatia maafa hayo, nyumba 109 zilihitaji kujengwa upya kwa haraka kwa kuzingatia athari hizo, na kwa upendo wake, Mhe. Rais  alitoa maelekezo ya kujenga nyumba bora na za kudumu katika eneo salama kwa waathirika waliopoteza makazi yao na kusisitiza kuwa, ujenzi huu ni ishara ya kujali, upendo na dhamira ya Serikali ya kuendelea kuwa pamoja na wananchi hususani wakati wa shida.



Hata hivyo, Mhe Rais Dkt. Samia alitoa fedha, kiasi cha shilingi Bilioni 1.38 kwa ajili ya kuweka huduma za kijamii ikiwemo umeme, maji na barabara za uhakika, kwa lengo la kuhakikisha kila nyumba inafikiwa na huduma hizo muhimu.



Awali, Mhe.Majaliwa amewaagiza viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanan'g, kuratibu zoezi la ugawaji wa viwanja vya ziada vilivyopo katika eneo hilo ili kuendeleza eneo hilo liwe na wakazi mchanganyiko sio wale walioathirika peke yao.



 “Tunataka eneo hili lisitambuliwe kama makazi ya waathirika, bali kijiji rasmi chenye huduma zote muhimu za kijamii na liwe kielelezo cha maboresho ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wote"


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa