• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WACHEZAJI WA ZAMANI WAKUMBUKWE-RC KIMANTA

Posted on: May 7th, 2021


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Iddi Hassan Kimanta amekabidhi kiasi cha shilingi Milioni 11 kwa vituo vya kulelea watoto yatima na kwa Bw.  Allan Shomari,  mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu  aliyewahi kuchezea timu za General Tyre  na Yanga.

Makabidhiano ya vituo vya watoto yatima yamefanyika ofisini kwa Mkuu wa Mkoa ambapo Kituo cha watoto yatima kinachosimamiwa na Msikiti wa Masjid Senta kimepatiwa shilingi Milioni 5 na kituo cha watoto walemavu kilicho chini ya Kanisa Katoliki Monduli(St.John Paul Rehabilitation Center) kimepatiwa shilingi Milioni 5.

Mhe. Mkuu wa Mkoa  alifika pia nyumbani kwa mchezaji wa zamani  wa Yanga, Bw. Allan Shomari na kumkabidhi shilingi Milioni Mhe. Kimanta aliahidi  pia kutoa mchango binafsi wa shilingi laki 5 kwa Bw. Allan Shomari.

Mhe. Kimanta amesema fedha hizo alizokabidhi zimetolewa na Shirikisho la  Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kutokana na mapato yaliyopatikana kwenye mechi ya Ngao ya Hisani  kati ya timu za Simba na Namungo iliyochezwa Jijini Arusha katika  uwanja wa Sheikh Amri Abeid tarehe 30 Agosti, 2020.

 Mhe. Kimanta ameviasa vituo hivyo vya watoto kuhakikisha  fedha hizo zinatumika kwa maendeleo ya vituo vyao na si vinginevyo.

Mhe. Kimanta ameishukuru TFF kwa mchango huo wa kuwasaidia watoto wa vituo hivyo na kwa msaada walitoa kwa aliyekuwa mchezaji  wa zamani wa Timu ya Yanga, Bw. Allan Shomari.

Mhe. Kimanta ametoa  rai kwa wadau wengine kujitokeza kuvisaidia vituo vya watoto yatima na wenye ulemavu na pia kujitokeza  kumsaidia  Bw. Allan  Shomari ambaye ni mlemavu wa macho.

Akizungumza kwa niaba ya  TFF,  Mwenyekiti wa TFF Mkoa wa Arusha Bw.  Zakayo Mjema amesema  fedha hizo zimetolewa kwa vituo vya watoto yatima kama  mchango  wa TFF kwa jamii na ni imani yake kuwa vituo hivyo vinaweza kuzalisha wachezaji wazuri wa baadae kwa manufaa ya Taifa letu.

Bw. Mjema ameongeza pia kuwa michezo ina fursa mbalimbali ikiwemo ajira kwa vijana na wao kama TFF Mkoa wa Arusha wataendelea kutoa misaada kwa watoto hao ikiwemo kuwapatia mipira ya kuchezea.

Ametoa wito kwa wadau wengine kuwasaidia wachezaji wa zamani kama walichofanya kwa Bw. Allan Shomari kwa vile bado wapo wengi mitaani wanaohitaji  msaada kama huo.

Akitoa neno la shukrani, Bw. Allan Shomari  ameushukuru uongozi wa TFF  na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Kimanta kwa msaada huo waliomkabidhi ambao utamsaidia hasa kwenye matibabu yake ya Macho.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa