• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WAFANYABIASHARA WADOGO WATAKIWA KUKUBALIANA NA MABADILIKO YANAYOTOKANA NA MAENDELEO YA KIUCHUMI....

Posted on: October 18th, 2023



Na Elinipa Lupembe

Wafanyabiasha wadogo Jiji la Arusha, wametakiwa kukubaliana na mabadiliko ya kiuchumi yanayotokea kwa kuwa ni mabadiliko yoyote lazima yanakuja na matokeo hasi ambayo huathiri sehemu na baadhi ya watu.

Hayo yamesemwa na mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella wakati wa mkutano wa hadhara uliowakutanisha wafanyabiashara wa soko Kilombero, uliofanyika kwenye eneo la Sokoni hapo ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kukagua utekelezaji wa shughuli za maendeleo Jiji la Arusha.

Mhe. Mongela amesema hayo mara baada ya kusikiliza na kutatua kero za wafanyabiashara hao wadogo waliolalamikia ubovu wa miundombinu ya barabara za Jiji kwa baadhi ya maeneo, kuhamisishwa mara kwa mara, uchakavu wa soko hilo pamoja na  mpango wa kuhamishwa stendi ya Daladala eneo la Kilombero .

Akijibu kero hizo, Mhe. Mongella ameweka wazi mpango wa serikali ya awamu ya sita ni kutekeleza awamu ya pili ya mradi mkakati wa kuboresha Miji na Majiji - TACTIC, ambao Jiji la Arusha ni miongoni mwa majiji yaliyopata neema hiyo, mradi unaotekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia.
 
Ameitaja miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa kiwango cha lami barabara za kuingia na kutoka jijini, ujenzi wa soko la Kisasa stendi ya Kilombero, ujenzi wa stendi ya Daladala, ujenzi wa Standi kubwa ya mabasi yaendayo mikoni, ujenzi na soko la kisasa la Machinga eneo la stendi kubwa, miradi ambayo kimsingi yataathiri baadhi ya maeneo na baadhi ya watu.

Amewataka wafanya biashara hao kukubalina na mabadiliko yanayokuja na kuondoa hofu kwamba watakosa wateja, mabadiliko hayo yana lenga kukuza sekta ya uchumi wa mkoa wa Arusha na Tanzania kwa ujumla wake hivyo ni vema kujiandaa kuyapokea, hivyo wafanyabiasha kukubali na kujiandaa kisaikolojia kuendana na wakati.

"Hapa ilipo stendi ya Daladala linajengwa soko la kisasa la Machinga, soko ambalo nyinyi wafanya biasha ndio mtafanya biashara humo, stendi itahamia nje ya mji na Daladala zitapita katikati ya Jiji kushusha abaliria tuu, ilikupungumza msongamano wa magari, ambao ni kero kwa wananchi na unachelewesha shughuli nyingi" Ameweka wa Mhe. Mongella.

Aidha ameuagiza uongozi wa Jiji la Arusha kuweka miundombinu ya taa kwenye soko la Kilombero ili wafanyabiashara waendelee kufanya biashara mpaka usiku na kuachana na kufunga saa 12, jambo ambalo linazorotesha uchumi hoja ambayo ilitolewa na mfanyabiashara kijana Andrea Thomas

#arushafursalukuki
#KaziInaendelea


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa