• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

*WAHIFADHI MNA DHAMANA YA KULINDA RASILIMALI ZA TAIFA- RC MAKALLA...

Posted on: September 19th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla amewataka Watumishi na Viongozi wa Mamlaka za hifadhi za Taifa zilizopo Mkoani Arusha kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kwa uzalendo, wakitambua kuwa wanayo dhamana kubwa ya kulinda rasilimali za nchi na uendelevu wa Vivutio vya Utalii vilivyopo Arusha.


CPA Makalla ameyasema hayo leo Jumamosi Septemba 20, 2025 Mto wa Mbu Karatu kwenye Makao Makuu ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, alipokutana na kuzungumza na Menejimenti ya Shirika la hifadhi ya Taifa TANAPA, akiwataka pia kuwa Mabalozi wazuri wa kusukuma mbele jitihada za Rais wa Awamu ya Sita Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kukuza utalii wa Mkoa wa Arusha na Tanzania.


"Nyie ni mabalozi wetu wazuri na tunawaamini, hakikisheni mnalinda hifadhi tulizonazo, mkitimiza majukumu yenu kwa uadilifu na uzalendo kwa nchi yenu. Utalii ni matokeo ya uhifadhi, tuunge Mkono jitihada za Mhe. Rais ambazo zimetusaidia kuwa na Ongezeko kubwa la Idadi ya watalii kwenye Hifadhi tulizonazo." Amesema Mhe. Makalla.


Aidha kando ya kusisitiza usimamizi wa sheria na Mipaka ya hifadhi kwa uadilifu na uzalendo Mkubwa, CPA Makalla pia ameahidi ushirikiano kwa wahifadhi hao, akibainisha pia umuhimu wa kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu uhifadhi na utalii pamoja na kuendeleza mahusiano mema na jamii zinazozunguka hifadhi za Utalii zilizopo kwenye Mkoa wa Arusha.


Awali katika maelezo yao, Mkuu wa hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara Yustina Kiwango na Witness Shoo, Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Arusha wameeleza kuongezeka kwa Idadi ya watalii kwenye hifadhi zao, suala lililoongeza mapato ya serikali na kukuza uchumi wa Mkoa wa Arusha, wakisema tija hiyo imepatikana zaidi kutokana na filamu za The Royal Tour na Amaizing Tanzania, zilizoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO MTIHANI WA UTAMIRIFU (MOCK) 2025 DARASA LA SABA (VII)- MKOA WA ARUSHA June 07, 2025
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKALLA: UFUNGUZI TAWI LA CRDB NAMANGA UTACHOCHEA BIASHARA NA UCHUMI WA WANANCHI WA MPAKANI ..

    September 26, 2025
  • RC MAKALLA ATAKA MPANGO MKAKATI WA UTALII UKIJUMUISHA FURSA NA MAANDALIZI YA AFCON 2027...

    September 25, 2025
  • WANANCHI WALIOLALAMIKIA MGAO WA MAJI WAFURAHIA UJENZI WA TENKI JIPYA LA MAJI...

    September 24, 2025
  • RC MAKALLA: ARUSHA ITAENDELEA KUWA NA AMANI SASA NA HATA  BAADA YA UCHAGUZI...

    September 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa