• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI ARUSHA WAJITOKEZA KWA WINGI  WIKI YA HUDUMA RASMI ZA KIFEDHA KUPATA ELIMU YA HUDUMA HIZO..

Posted on: November 24th, 2023

Na Daniel Gitaro



Ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma za kifedha, Wananchi wa Mkoa wa Arusha, wamejitokeza kwa wingi kutembelea na kupata elimu ya huduma za kifedha kwenye mabanda mbalimbali ya watoa huduma hizo na kuvuka lengo lililokuwa limewekwa la kufikia wananchi elfu nane.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Felician Mtahengerwa alipokuwa akihitimisha maonyesho hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John V.K. Mongella, ambapo wananchi zaidi ya elfu kumi walijitokeza kushiriki maonyesho hayo na kupata elimu ya huduma za kifedha.

Aidha, amesema kuwa, utoaji wa elimu hiyo utasaidia wananchi kupata uelewa juu ya elimu ya fedha na kufikia lengo lililowekwa la kufikia asilimia 80 ya wananchi kufikiwa na huduma hiyo ifikapo mwaka 2025.

“Ni matumaini yangu kuwa elimu iliyotolewa kupitia maadhimisho haya itawawezesha wananchi walio wengi kutumia huduma za kifedha zilizo rasmi na kwa ufanisi ili kuboresha maisha yenu kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi”. Amesema.

Kwa upande wake Kamishina wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha Dkt. Charles Mwamwaja amesema kuwa lengo kuu ya maadhimisho hayo ni kutoa elimu kwa wananchi kuhusu utumiaji wa huduma za kifedha, jambo ambalo limefanyika wakati wa maadhimisho hayo.
Ameongeza kuwa, Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na wadau mbalimbali na watoa huduma za kifedha, wataendelea kutoa programu hizo za mafunzo ka kutumia njia na mbinu mbalimbali na hatimaye kuwafikia wananchi wengi Zaidi.

“Tunaamini elimu hii imewafikia watanzania wengi, lakini elimu inakuwa ina maana sana kama itakusaidia kubadilisha maisha yako na kubadilisha namna ambayo ulikuwa ukiishi hapo awali kabla ya kupata elimu, hivyo ni vyema wananchi mkazingitie yale mliyoyapata hapa kwa manufaa ya shughuli zenu za kimaendeleo”.

Hata hivyo, baadhi ya watoa huduma za kifedha walioshiriki kwenye maonyesho hayo wamethibitisha uwepo wa uhaba wa elimu ya masuala ya kifedha kwa wananchi walio wengi hali inayosababisha kujiingiza kwenye mikopo  inayowaumiza.

Nao baadhi ya wananchi waliohudhuria wakati wa kilele cha maadhimisho hayo wamesema wamefurahishwa sana huduma hiyo kwani wamepata elimu ya msingi sana itakayowasaidia kuweka akiba na kutengeneza faida kutokana na shughuli zao za maendeleo.

“Maonyesho haya yamekuwa na manufaa makubwa sana kwetu hasa wakazi wa Arusha kwasababu tumepata elimu mbalimbali kuhusu masuala ya kifedha, kukopa na kuweka akiba, namna ya kukua kiuchumi kupitia vikundi vidogo vidogo pamoja na Sheria za kifedha”. Amesema Lazaros Laizer.

Awali, maonyesho ni ya tatu kufanyika kitaifa, na kuleta mafanikio makubwa Zaidi ya maonyesho yliyofanyika hapo awali Jijini Dar-es-salaam na jijini

#arushafursalukuki

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa