• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI LAJA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KUWAEPUSHA WATOTO KUISHI 'MAGETO'....

Posted on: April 5th, 2024

Na Elinipa Lupembe

Wananchi na wakazi wa Kijiji cha Laja kata ya Ganako, wilaya ya Karatu, wamemshukuru Rais Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwajengea shule mpya ya Sekondari Laja, shule iliyowapushia gharama za kuwapangia watoto wao vyumba maarufu kama 'mageto' wakati wakienda kusoma kata za mbali.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, wananchi hao wamesema kuwa, Serikali  kujenga shule katika eneo lao, shule ambayo licha ya watoto wao kupata elimu, wamekiri kuwapunguzia wazazi mzigo wa gharama za kuwapangia vyumba (mageto), miaka yote  wakiwa shuleni

"Ilikuwa mtoto akipangiwa sekondari, tulilazimika kuwapangia vyumba  karibu na shule huko Laansey, ilikuwa na gharama kubwa pamoja na usalama mdogo kwa watoto, zaidi wazazi wengi hawakuweza kumudu gharama hizo na watoto kulazimika kutembea umbali mrefu" Wamesema wananchi hao.

Wamesema kuwa, watoto wao wamepata fursa ya kusoma ndani ya eneo lao, wakati hapo awali walitembea zaidi ya Km 10 -16 kwenda na kurudi shuleni, jambo lililosababisha utoro kwa wanafunzi sambamba na baadhi kuacha shule kutokana na utoro na mimba za utotoni kwa wasichana.

Rehema Matley Amey, amesema kuwa, Serikali ya mama Samia imefanya miradi mingi katani hapo, imejenga shule ambayo imewaondolea kero na changamoto watoto ambao walitembea umbali mrefu huku kipindi cha mvua wakikosa masomo kutokana na makorongo kujaa maji lakini sasa changamoto hizo hazipo, shule imejengwa na daraja limejengwa hakuna tena watoto kukosa masomo.

"Tunaishukuru mama Samia kupitia TASAF, ilianza kwa kujenga daraja na shule ikafuata, watoto wetu waliishi kwenye nyumba za kupanga mitaani 'mageto' wakati wanasoma Kansay huku watoto  wakiishi bila usimamizi jambo ambao wasichana walifanyiwa vitendo vya ukati na wengine kuacha masomo kwa kupata mimba za utotoni" Amesema Mama Rehema

Hata hivyo, wanafunzi wa shule ya Sekondari Laja, hawakuwa nyuma, wamemshukuru Mama Samia kwa kuwajengea shule, huku wakijipongeza na kujivunia kwa kuanzisha shule mpya na kumuomba Mheshimiwa Rais kuwajengea Hosteli kwa kuwa bado wapo wanafunzi wanaotoka mbali na shule ilipo.

Emmanuel Fanueli, amesema kuwa anajivunia kwa kuwa wanafunzi wa kwanza kwa kuanzisha shule hiyo ya Laja, nakumuahidi Mama Samia kusoma kwa bidii huku akimuomba Mama Samia kuwajengea Hosteli ili wanafunzi waweze kulala shuleni.

"Tunamshukuru rais Samia ametujali watoto wa kike Laja, wengi waliacha shule kutokana na mimba za utotoni lakini  uwepo wa shule hii hapa jirani, tunamuadi Rais kusoma kwa bidii na kuwa Mwalimu" Amesema Elizabeth Mathay Niima.

Mkuu wa shule ya Sekondari Laja, Mwl. Daniel Awey Panga, amesema kuwa shule hiyo imejengwa kwa gharama ya shilingi milioni 333.3 fedha kutoka Serikali Kuu kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF - OPEC IV), shule ambayo tayari wanafunzi 25 wa kidato cha kwanza, wameanza masomo mapema Januari 2024.


#ArushaFursaLukuki

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA AFUNGUA MKUTANO WA 33 WA WAKUU WA MAJESHI YA ULINZI (SADC).

    May 30, 2025
  • SAMIA MOTOCROSS CHAMPIONSHIP KUREJEA MSIMU WA PILI JULAI 12, 2025

    May 27, 2025
  • MKOA WA ARUSHA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUBWA WA WAKUU WA MAJESHI WA SADC

    May 25, 2025
  • UJENZI WA UWANJA WA AFCON ARUSHA SIO MICHEZO TU, NI FURSA YA KIUCHUMI

    May 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa