• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI WAHAMASISHWA ULAJI WA MBOGAMBOGA

Posted on: January 15th, 2019

Katibu tawala wa Mkoa wa Mkoa wa Arusha Richard Kwitega, amesema utapiamlo sasa basi kwa mkoa wa Arusha, kwani  wakulima na walaji wa mbogamboga wameungana pamoja kwa lengo la kuhimiza ulaji mzuri wa mbogamboga.

Ameyasema hayo alipokuwa akifungua warsha ya siku moja ya wadau wa uzalishaji na ulaji wa mbogamboga katika halmashauri ya Jiji la Arusha,halmashauri ya Arusha na halmashauri ya Meru.

Kwitega amesema, lishe ina muunganiko wa uzalishaji na uwandaaji wa vyakula tunavyotumia kila siku katika maisha ya mwanadamu.

Hata hivyo amesema,mpango wa kutokomeza utapiamlo kwa mkoa wa Arusha umelenga hasa kwa makundi matatu maalumu; Watoto,Wagonjwa,Wanawake walio katika umri wa kuzaa na Wazee.

Kwitega amesisitiza zaidi kuwa utapiamlo unasababishwa na upungufu wa Wanga, Vitamin, Madini,Unene kupita kiasi na wathirika wakubwa ni watoto wenye umri chini ya miaka 5 na wanawake walio katika umri wa kuzaa.

Mbali na hayo amesema changamoto kubwa zinazosababisha hali ya utapiamlo kuongezeka katika Mkoa wa Arusha ni pamoja na hali ya umaskini kwa jamii,ukosefu wa elimu ya kutosha kwa jamii.

Pia utashi na uwajibikaji wa baadhi ya viongozi, wananchi kuwa tegemezi na mabadiliko ya tabia nchi.

Hivyo elimu sahihi kwa wananchi itasaidia kutokomeza kabisa tatizo la utapiamlo na kupelekea kuwa na kizazi chenye afya bora na kuweza kukuza uchumi wa nchi kwani uzalishaji nao utakuwa.

Mganga mkuu wa Mkoa Wedson Sichalwe amesema, jitihada za pamoja bado zinaitajika kati ya serikali, wadau na wananchi katika kuhakikisha utapiamlo unatokomezwa kabisa katika mkoa wa Arusha.

Sichalwe amesema kama Mkoa utaendelea kushirikiana kwa karibu sana na wadau na wakulima wa mbogamboga katika kuhakikisha elimu sahihi inawafikiwa walaji na hata wakulima wenyewe juu ya uzalishaji na ulaji wa mbogamboga.

Akisoma taarifa fupi ya mradi wa uzalishaji na ulaji mbogamboga Mratibu wa Mradi bwana Peter Bayo kutoka taasis ya ANGONET amesema, mradi huo kwa kuanzia utakuwa katika halmashauri ya Jiji la Arusha, halmashauri ya Arusha na halmshauri ya Meru.

Amesema takribani 93% ya wananchi hawatumii mbogamboga katika milo yao na hali hii kupelekea kiwango cha utapiamlo kuwa juu.

Mradi huo unatarajia kuwafikia takribani watu 1000 kila wilaya na hasa kwa wakulima wenyewe wa mbogamboga na wanafunzi katika shule za msingi kwa kuwafundisha kuanzisha vitalu vya mbogomboga katika maeneo ya shule zao.

Peter amesema, mradi huo una miezi 3 tokea kuanzishwa na takribani kata 3 za kila wilaya zitahusishwa na mradi huu na wanatarajia zaidi ya wakulima 3000 watanufaika nao.

Amesema mradi huu wa uzalishaji na ulaji wa mbogomboga utahusisha zaidi utoaji elimu sahihi ya lishe na ulaji wa mbogamboga, kuanzisha bustani za mbogamboga katika mashule,watafanya warsha mbalimbali za uhamasishaji,utayarishaji na upikaji bora wa mbogamboga.

Mradi wa uzalishaji na ulaji wa mbogamboga umeanzishwa rasmi katika Mkoa wa Arusha na taasis ya ANGONET,TAHA  na RULIDE & COMECA kwa kushirikiana na serikali ya Mkoa wa Arusha ili kuimarisha hali ya lishe na kutokomeza utapiamlo.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa