• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WATAALAM WA MIFUGO WATAKIWA KUTUMIA MIONGOZO KATIKA KUTIBU WANYAMA...

Posted on: November 17th, 2023

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amewataka wataalam wa Afya ya Binadamu na Mifugo kutumia miongozo mipya kutekeleza majukumu yao ili kuzuia tatizo la usugu wa vimelea dhidi ya dawa na kuepuka matumizi mabaya yasiyozingatia utaratibu kutoka kwa wataalam wa afya ya binadamu na wanyama.


Mhe. Ulega ametoa maagizo hayo wakati akifungua kongamano la tatu la kuzuia Usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa, lililofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano Hoteli ya Mount Meru.


“Matumizi mabaya ya madawa yamesababisha ongezeko la vimelea vya magonjwa ambavyo havitibiki kwa urahisi kwa kutumia dawa zilizopo sokoni hali ambayo inasababisha vifo Zaidi ya laki saba kila mwaka”. Amesema Mhe. Ulega.


Naye Mkuu wa Mkoa Wa Arusha, Mhe. John V.K. Mongella, ametumia fursa hiyo kuomba Kongamano kama hilo kufanyika mara kwa mara katika ngazi za mikoa na Serikali za Mitaa ili elimu hiyo iweze kuwafikia wataalam wote na kupunguza changamoto hiyo.


“Sisi ndio tunakaa na hawa wananchi ambao ndio watumiaji wa dawa hizi na wahanga wa vimelea sugu kutokana na matumizi ya dawa, hivyo ni vyema viongozi wa ngazi za Mikoa na Wilaya kupata elimu hii kwa usahihi na kuipeleka kwa wananchi wengine kwenye ngazi zote”. Amesema Mongella.


Aidha, Mkurugenzi wa Idara ya Mifugo Prof. Hezron Mnonga wakati akiwasilisha mkakati wa Serikali wa kuendeleza mapambano ya kuzuia usugu dhidi ya vimelea vya dawa, amesema kuwa Tanzania ni moja kati ya mataifa yote duniani yanayotumia Mfumo wa Afya shirikishi unaolenga kupunguza changamoto hiyo.


“Nchi yetu tumebahatika kuanza kushughulikia hili tatizo la usugu wa vimelea dhidi ya dawa tangu mwanzi mwa mwaka 2011 na sasa malengo yetu katika kipindi hiki ni kushuka chini mpaka kwenye ngazi za vijiji na vitongoji tofauti ilivyokuwa kwenye mpango mkakati tulionao ambao ulijikita kwenye ngazi ya Taifa”.


Hata hivyo, kongamano hilo limeambatana na uzinduzi wa muongozo mpya kwa wataalam wa afya ya binadamu utakaowawezesha kutoa huduma za tiba kwa usahihi na kusaidia kupunguza changamoto hiyo kwa kiasi kikubwa.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa