• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI MCHENGERWA AAGIZA TAMISEMI KUJENGA MADARASA NANE SHULE YA SEKONDARI KIUTU ARUSHA.

Posted on: October 2nd, 2024


Na Elinipa Lupembe 



Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa ameahidi kuomba fedha kwa Mheshimiwa Rais,  Dkt. Samia Suluhu Hassan kwaajili ya kuongeza nguvu za Ujenzi wa madarasa nane kwenye shule ya Sekondari Kiutu, Halmashauri ya Arusha wilaya ya Arumeru Mkoa wa Arusha. 



Mhe. Mchengerwa ametoa ahadi hiyo mapema leo Oktoba 02, 2024, alipotembelea shuleni hapo kwa lengo la kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari Kiutu, iliyojengwa na Serikali kwa gharama ya shilingi milioni 800 kupitia programu ya kuboresha miundombinu ya shule za sekondari nchini (SEQUIP) na kuahidi kuongeza fedha za kujenga vyumba 8 vya madarasa shuleni hapo.



Mhe. Mchengerwa amefurahishwa na hali ya maendeleo ya shule hiyo yenye jengo la ghorofa tatu ikiwa na takribani wanafunzi 500, na kumuagiza Katibu Mkuu wa TAMISEMI na Mkurugenzi wa Elimu kufika kwenye Shule hapo na kufanya tathmini ili kufahamu gharama za ujenzi wa madarasa hayo nane ambayo wizara ya TAMISEMI itayajenga.



Hata hivyo Mhe. Mchengerwa amewapongeza wananchi, uongozi wa wilaya na halmashauri na mkoa chini ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Paul Chritiana Makonda, kwa kuwaunganisha wananchi na kuwafanya kujitolea na kuchangia shughuli za Maendeleo, kwa manufaa ya Umaa huku akitoa pongezi nyingi kwa Diwani wa kata ya Kiutu Mhe. Malaki Malambo kwa kutoa eneonlake la Mita za mraba 6,400 na kujenga shule hiyo ya Kiutu.



"Ninawaponheza wananchi wote, watalamu, mkurugenzi, Mbunge Baraza la Madiwani kwa ushirikiano wenu kwa manufaa ya Umma, nikupongeze Mheshimiwa Diwani kwa kjitoa kwa ajili ya wananchi wako, niwaombe Madiwani wote nchini kuiga mfano huu wa kujitoa kwa hali na mali kwa ajili ya wananchi waliowachagua" Amesema 



Awali Mhe. Mchengerwa yupo mkoani Arusha kwa ziara ya kikazi ikiwa ni awamu yake ya pili ya ziara Mkoani hapo yenye lengo la kukagua hali ya utekelezaji wa shughuli wa maendeleo ikiwemo mirafi pamoja na kuzungumza na wananchi kwenye mikutano ya hadhara.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa