• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI MCHENGERWA AAHIDI UCHAGUZI WA HAKI NA UWAZI KATIKA SERIKALI ZA MITAA

Posted on: November 16th, 2024


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Mohamed Mchengerwa ameeleza kuwa, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27,2024 utakuwa wa haki, uwazi.



Pia, uchaguzi huo utazingatia misingi ya umoja na mshikamano, pamoja na falsafa ya R4 za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.



Waziri Mchengerwa amesema kuwa, Ofisi ya Rais TAMISEMI ilianzishwa na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa lengo la kusogeza maamuzi karibu kabisa na wananchi.



Amefafanua kwa kusema kwamba, uchaguzi wa serikali za mitaa ni tofauti na uchaguzi mkuu, kwani mfumo wake unalenga wakazi ambao wanatambuana katika maeneo yao. 



Utambuzi huu wa wakazi unategemea wenyewe wakazi wa eneo husika.



Amesema hayo Novemba 12, 2024 jijini Dar es Salaam wakati akifungua semina ya wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini.



Waziri Mchengerwa ameendelea kusema kwamba Bunge halikufanya marekebisho ya Ibara ya 145 na 146 ya katiba, wala tafsiri ya sheria inayosimamia uchaguzi wa serikali za mitaa.



Hata hivyo, Bunge lilifanya marekebisho ya sheria inayosimamia mchakato wa chaguzi zinazoratibiwa na Tume Huru ya Uchaguzi.



Vilevile Waziri Mchengerwa ameeleza kwamba, kumekuwa na propaganda za kisiasa kuhusu hali ya uchaguzi wa serikali za mitaa, ambapo amedai zinatolewa na baadhi ya watu ambao hawakuwa wamejiandaa vyema.



Amesema kuwa, uchaguzi huo ni shirikishi, na maandalizi yamehusisha vyama vyote vya siasa kwa njia ya vikao na mashauriano ya mara kwa mara na wadau wa vyama vya siasa.



Kuhusu kutotumika kwa vitambulisho wakati wa uandikishaji, Waziri Mchengerwa amesema 



"Tungeweza kunyima haki za Watanzania walio wengi endapo tungeamua kuwa lazima kila mtu awe na kitambulisho ili aandikishwe. 



"Tunatambua kwamba wananchi wengi, hasa wanaoishi kwenye vitongoji na vijiji, hawana vitambulisho. 



"Hivyo, hatua hii imezingatiwa ili kila Mtanzania apate fursa ya kushiriki uchaguzi," amesema Mheshimiwa Mchengerwa.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa